Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-02-07

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aaah
Yaani niue albino ndio niwe tajiri, aaah hapana sitaki kuwa kwenye orodha ya wauaji, kama ni umaskini acha niwe, hata kama watu watasema nimeporomoka sawa tu,” alijisemea Kazim. [1]
aende
Wimbo huo ulimfanya aende katika Umoja wa Mataifa kumuaga Koffi Annan alipomaliza muda wake wa ukatibu mkuu wa umoja huo. [2]
akioza
Samaki mmoja akioza, wote wameoza. [3]
alifoka
Sasa huo si ujinga, picha ndio nini? Picha ndio dawa,” alifoka Kazim hali iliyomfanya waziri aendelee kufadhaika na kumueleza kuwa watakachokifanya ni kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari. [4]
alikuwa
KATIBU wa chama cha NCCR- Mageuzi wilayani Karatu, ambaye alikuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti Taifa wa chama hicho hivi karibuni, John Bura Dodo pamoja na wananchi wengine 469 wa Karatu juzi wamejiunga na Chama cha Mapinduzi CCM wilayani hapa. [5]
alipo
Msanii huyo mzawa wa Dar es salaam alianza kusikika Octoba 2006 na hakutegemea kama ndani ya miaka miwili angefika hapo alipo, lakini kwa sasa, anajivumia mafanikio makubwa, huku akishangaa jinsi alivyopokelewa haraka na jamii na kwa mikono miwili. [6]
alisoma
Siku moja baada ya kukutana na jamaa huyo alisoma taarifa kwenye gazeti moja kwamba kuna biashara kubwa ya kununua viungo vya albino kwa ajili ya machimbo ya madini na biashara ya uvuvi. [7]
ama
Kwa sababu, hafahamiki kama ni viongozi wale ambao wanachaguliwa katika mvumo wa uongozi ndani ya vyama ama ni wale waliochaguliwa na wananchi kwa taratibu za kiserikali kama vile rais, wabunge, madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji na vitiongoji. [8]
ambayo
Kina kalenda ambayo mtumiaji huweza kuiseti kwa jinsi anavyotaka. [9]
ameamua
Akizungumza katika mkutano huo, Dodo alisema ameamua kurejea CCM, kutokana na kupinga Udikteta wa Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia. [10]
ana
Kibaden alisema kuwa wachezaji wake wako vizuri na ana nafasi kubwa ya timu yake kurudi katika Ligi Kuu ya Vodacom kama ilivyokuwa msimu uliopita. [11]
anasema
Akifafanua, anasema wakati unapotafuta pesa ya kujikimu maisha hutakiwi kuchagua kazi ya kufanya wala kuwa na aibu, mradi kazi hiyo iwe ni halali. [12]
anataka
Hakusikilizi, anataka umsikilize. [13]
au
Vifaa hivyo vinatumika kurekodi sauti na vimethibitishwa kutokuwa na uwezo wa kupiga picha za mnato au video wala havina uwezo wa kusafirisha mawasiliano kwenda sehemu nyingine," alifafanua Mganga. [14]
badala
Naye Awila Silla, anaripoti kutoka Singida kuwa, vyama vya upinzani nchini vimetakiwa kuungana ili kuunda chama kimoja chenye sera, ili kuleta changamoto kwa chama tawala badala ya kuendeleza marumbano. [15]
bado
WAKATI Tanzania ikiwa bado haieleweki ni siasa ya aina gani inafuata Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amekata ukimwia na kuweka bayana kuwa, sera ya ujamaa na kujitegemea iliyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere ilipekechwa na kunguni. [16]
bali
Umaarufu wa Mwasiti si katika kuimba tu kama ilivyo kwa vijana wengi, bali hata kutunga nyimbo mbalimbali zenye kuelimisha, kuburudisha hata kuifahamisha jamii. [17]
biashara
Ukizipata fedha hizo, zifanyie biashara ili uendelee. [18]
bila
Katika mkutano huo pia Mwinyi alivaa sura ya ubaba wa taifa kama alivyofanya akiwa Mbeya Vijijini, alipowataka wapiga kura kuchagua kiongozi wanayeona anafaa bila kujali vyama, pale aliposisitiza ushirikiano baina vyama vyote vya siasa, akiwataka wana-CCM kuimarisha uhusiano na vyama vya upinzani. [19]
binadamu
Kuhusu Mgodi Bunlyanhulu kamati hiyo imesema kuwa Shirika la Misaada la Kanisa la nchi hiyo (NCA) lilifanya utafiti katika mgodi huo mwaka 1999 kuhusuhali ya haki za binadamu na kubaini ukiukwaji mkubwa wa haki hizo unaohusina na shughuli za madini. [20]
budi
Hali halisi ya mahakama zetu mnazifahamu si za kuridhisha nyingi zimechakaa na ziko hatarini kuanguka ili zisilete madhara kwa wafanyakazi hatuna budi kufunga mahakama hizo ili kunususuru maisha ya wafanyakazi wetu," alisema Mchome. [21]
bwana
Wiki kama mbili tatu zilizopita kiwanja kilikuwa kinondoni Morocco, unaona bwana, mahala panaitwa Zhonghua Garden, burudani ilikuwa ikipatikana pale, na kwa kuwa ni karibu na makazi ya watu bahati mbaya ikawa yaisha kama mapema hivi, ...si unajua raha ya burudani kukesha? Malalamiko yaelekea yalifika kunako, na habari mpya kwa wasioijua, hii hapa. [22]
cha
Muda wa kunasa sauti huweza kuanzia saa 18 hadi 300 huku kikitumia kiasi kidogo sana cha umeme au betri. [23]
chao
Aliwataka wafanyakazi wa shirika hilo kufanya kazi kwa bidii na kuepukana na migomo inayoweza kukwamisha utendaji na kwamba, kukiwa na matatizo watumie chama chao cha wafanyakazi kuyapatia ufumbuzi. [24]
dampo
Hata hivyo alisema Manispaa hiyo, imekuwa ikihamasisha watu kutotumia mifuko laini ya plastiki kutokana na kuwa kero na kushindwa kudhibitika katika mji ya Arusha hasa maeneo ya jirani na dampo kuu la Arusha. [25]
es
Wataalamu hao walitumwa kutoka Dar es salaam kwenda Dodoma kufanya uchunguzi wa kina juu ya vifaa hivyo, vilivyokutwa kwenye vyumba vya Dk Wilibrod Slaa (Chadema-Karatu na ) Mbunge wa Konde, Dk Ali Tarab Ali kwenye Hoteli ya Fifty Six, iliyopo jirani na jengo la Bunge. [26]
eti
Mimi nashangaa na huu uongozi wa Manispaa kutumia nguvu kupita kiasi kupambana na mifuko kwa kutunyanyasa sisi wananchi wa kawaida kwa madai eti wanataka mji wa Arusha uwe safi," alilalamika Mwajuma. [27]
fainali
Gazeti hilo lilisema kuwa Rwanda ina uwezo wa kuandaa fainali hizo, lakini kibarua hicho wanawaachia Cameroon na Kenya. [28]
filamu
Norah aliyasema hayo baada ya uzinduzi wa filamu yao mpya ya ‘Upande wa Pili Ndoa isiyo na Uaminifu’ iliyozinduliwa juzi kwenye Ukumbi wa Century Cinemax, Mlimani City. [29]
ghafla
Na wakati naangalia hivi nikasikia ghafla kama samaki wa chini wanaanza kuongea. [30]
haina
Nilitaka kutokwa na machozi nilipoona sehemu moja ya mahakama ya mkoa haina choo inabidi wafanyakazi wa kawaida waende kuomba kujisaidia ofisi ya TRA iliyoko karibu katika mazingira kama haya msitegemee mahakama zetu kufanya miujiza ya kutoa haki haraka," alisema. [31]
haja
Slaa hana haja ya kuogopa vitu hivyo kama yuko safi. [32]
hajui
Kauli hiyo ilionekana kumchanganya sana Kazim, akawa hajui la kufanya. [33]
hapo
Ziara hii ni nzuri kwa sababu, hapo kabla hatukuwa tukiifahamu Msumbiji jinsi wanavyocheza na wala kujua kama wana uwanja wa nyasi bandia. [34]
hasa
Ugunduzi zaidi wa wataalamu hao, Maganga alisema kuwa wamebaini vifaa hivyo vya elektroniki anaweza kuwa navyo mtu yeyote, kwa sababu vinauzwa kwenye masoko hasa kwenye nchi zinazoendelea. [35]
hatutaki
Sisi hatutaki, hatutaki lakini tutatupwa kama hao. [36]
hawezi
Sla alisema tukio hilo halijamuogopesha na hawezi kuikimbia hoteli hiyo kwa matatizo hayo. [37]
hayo
Pamoja na hayo, mtumiaji anaweza kuweka neno la siri kuhakikisha hakuna mtu mwingine anayeweza kukitumia, ikiwa ni njia salama ya kuhakikisha alichorekodi kinabaki salama. [38]
hayuko
Atataka umfanyie hiki umfanyie hiki lakini yeye hayuko tayari kwa lolote juu yako. [39]
hicho
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo katika mtandao wa internet, kifaa hicho ambacho hutumiwa na wataalamu wa ukachero, kina uwezo mkubwa wa kunasa sauti kwa muda mrefu, kulingana na aina ya kifaa hicho. [40]
hii
Mwinyi alisema kinachofanyika ni kama mcheza mpira na mtazamaji kwamba, wananchi tunaona makosa ya awamu hii, lakini ukweli ni kwamba makosa mengi yametokea katika awamu zilizopita. [41]
hiki
Kipengele hiki kinazua utata kwa sababu tafsiri halisi ya kiongozi wa siasa anayezungumziwa hafahamiki. [42]
hili
Matokeo yake, ndondi hizo hazina mwenyewe, kiasi kwamba maendeleo yoyote hayawezi kufikiwa kama shirikisho hili, BFT halina na viongozi au waliopo ni dhaifu na wanaojihusisha na matendo ya kihuni. [43]
hivi
Katika miaka ya hivi karibuni, wakazi wanaoishi jirani na Dampo la Arusha lilipo eneo la Murieti wamekuwa wakilalamikia kusambaa kwa mifuko hiyo hadi kwenye mashamba hata hivyo hali hiyo imetokana na dampo hilo kutengenezwa chini ya kiwango licha ya wafadhili na serikali kutoa mamilion ya fedha. [44]
hizi
Mwandishi wa habari hizi, jana alishuhudia mifuko mipya aina ya salfeti iliyopewa jina la Mambo vipi ambayo imeanza kuuzwa katika masoko ya Arusha na kuonekana kuungwa mkono na baadhi ya maafisa wa manispaa hiyo. [45]
hizo
Juzi juzi tu alikwenda Zanzibar na kuwatangazia wananchi kuwa ataongeza fedha hizo. [46]
hospitali
Alihangahaika kwenye hospitali nyingi bila mafanikio. [47]
huduma
Awali Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, John Tipe alisema, wilaya ya Karatu kwa kiasi kikubwa imetekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa kuhakikisha kila Kata inakuwa na sekondari, huduma za afya na huduma bora za maji. [48]
huko
Kamati pia inatambua kazi ya utafiti iliyofanywa na Shirika la misaada la Kanisa la Norway (NCA) kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu unaohusiana na shughuli za madini huko Bulyanhulu, Tanzania," ilisema. [49]
huo
Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Samson Kassala pamoja na kuthibitisha kuwa ofisi ya DCI imetuma wataalamu hao kwenda kufanya uchunguzi, lakini hakutaja uchunguzi huo umeshabaini nini wala utakamilika lini. [50]
huu
Aliwakumbusha pia kujiandaa na chaguzi zijazo, Napenda kuwakumbusha wana CCM wenzangu kwamba msisahau kuwa tuna uchaguzi mwaka huu wa Serikali za Mitaa na mwakani tuna uchaguzi mkuu. [51]
huwa
Slaa huwa anatumia chumba hicho kila inapotokea vikao vya bunge na amekuwa na mhudumu ambaye amekuwa akifanya usafi katika chumba hicho na kila Jumapili huwa anaondoa godoro na kulisafisha. [52]
huyo
Lakini rais huyo mstaafu tangu mwaka 1995, aliwatupia wapinzani dongo la kushindwa kwao kukua: "tangu wakati huo wamebaki na asilimia 20 zao na CCM imebaki na ushindi wake wa asilimia 80," alisema. [53]
ijayo
KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Marcio Maximo amesema kimsingi hawezi kuwazuia wachezaji wa Yanga kwenda kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Etoile d’Or Mirontsy ya Comoro wiki ijayo kwani suala hilo ni la kiutawala zaidi. [54]
ikawa
Milango na madirisha ikafunguliwa ikawa rukhsa," alisema Mwinyi huku akishangiliwa na wanachama wa CCM waliokuwa wamefurika katika uwanja huo. [55]
iko
Mbali na hilo, Maximo alisema timu yake iko vizuri na anajivunia kwenda Ivory Coast na timu ambayo si ya kubeza. [56]
ila
Mama huyo anasema hapatani na wahuni, ila anachokitafuta yeye ni kuhakikisha anapata pesa kwa ajili ya kuwatunza binti yake ambaye ameanza darasa la kwanza mwaka huu, na wazazi wake walioko Iringa. [57]
ile
Waliozoea uongozi wa kununua sheria ile ya bunge itawabana vilivyo na hiyo ni sheria ya nchi wala sio ya chama na itatusaidia sana kuondoa kansa inayokula chama chetu na imekuwa ikiwaudhi watu wengi wakiwamo wa vyama vya upinzani,"alisema Rais Kikwete. [58]
ili
Hata hivyo, Mganga alisema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo, ili kujua aliyehusika na vifaa hivyo. [59]
ina
Kwa mujibu wa taarifa ya timu ya utafiti ya serikali ya Norway ambayo Mwananchi Jumapili ina nakala yake Kampuni ya Barrick Gold Corporation ya Canada yenye inayomiliki na kuendesha migodi nchi zaidi ya 26 duniani ikiwamo Tanzania imehusishwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira katika nchi mablimbali hivyo kuhatarisha fedha za serikali ya nchi hiyo. [60]
ingawa
Na ingawa wote walikuwa wananuka, kila mmoja alikuwa anamnyooshea kidole mwenzie kwa nini ananuka huku akinuka mwenyewe. [61]
iwe
Nawaombeni muachane na migogoro ambayo inasababisha migomo kwa kutumia vyama vyenu vya wafanyakazi, kugoma iwe hatua ya mwisho endapo mambo yakishindikana," alisema Kaboyonga. [62]
kabisa
Mmeyaona mambo mazuri kabisa yaliyotajwa kama mafanikio ya utekelezaji wa sera za CCM," alisema. [63]
kadhaa
Kusimama kwa ligi hiyo kumetokana na timu kadhaa, zikiwamo Yanga, Simba, Mtibwa kuwa na wachezaji wengi katika kikosi cha Stars. [64]
kamati
Taarifa hiyo ya serikali ya Norway imesema kamati ya Maadili ya mfuko huo wa penseni wa serikali iliamua kufanya utafiti huo kubaini iwapo Barrick itahatarisha fedha zake baada ya kubainika imehusika na tuhuma mbalimbali za uharibifu wa mazingira katika nchi tofauti. [65]
kambi
Mara baada ya tangazo hilo na Makinda kutangaza kuwa muswada umepita, wabunge wa CCM waligonga meza kwa ishara ya kuafiki na wakati huo huo, maneno mbalimbali ya kuzomea kutoka sehemu walikokuwa wamekaa wabunge wa kambi ya upinzani yalisikika. [66]
kana
Kutokana na kashfa hiyo, BFT imekuwa kana kwamba hapo na haitoi tena mchango katika kuendeleza mchezo huo. [67]
kati
Alisema kati ya kampuni 916 zilizokopa fedha hizo tayari kampuni yake imezifikia kati ya kampuni 300 na 400 na kubainisha kwamba, miongoni mwa kampuni hizo zipo zilizoanza kulipa madeni na nyingine zimegoma. [68]
katiba
Kwa sababu hiyo, Marmo alisema muswada huo hauwezi kupingana na katiba, hivyo kama wapinzani wanataka wabadilishe kipengele hicho, itabidi kwanza yawepo mabadiliko ya katiba ili kuondoa ukinzani na sheria mama. [69]
kibao
Nimewahi kupelekwa kituo cha polisi siku moja kutokana na mtu ambaye alikuwa anadaiwa nauli kunigeuzia kibao kuwa nimemuibia, niliteseka, lakini kwa vile sikuwa nimemuibia, polisi waliniachia," anasema na kuongeza kuwa matukio ya namna hiyo tayari ameyazoea. [70]
kikosi
Katika majina hayo, wachezaji wa Ghana, Nigeria na Cameroon ndiyo waliotawala katika kikosi hicho. [71]
kile
Watu waligawana sawa kile walichozalisha kwa usawa. [72]
kirafiki
Timu hizo zimewahi kucheza mara moja timu katika mechi ya kirafiki, Agosti 1999, wakati bao la Gabriel Okolosi wa Nigeria liliiwezesha kushinda 1-0 mjini Maputo. [73]
kocha
Yanga kuondoka sijapata taarifa za TFF, nasema ni la kiutawala zaidi," alisema kocha huyo. [74]
kote
Tunasema kuwa ukiacha soka, mchezo wa ndondi kote duniani ndio unaofuatia kwa kupendwa zaidi na watu wengi, lakini hapa kwetu ni tofauti kwa sababu ya viongozi wabovu. [75]
kuanza
Kabla ya kuanza kufanya naye mazungumzo naye mwandishi wa makala haya alilazimika kupanda gari lake ili kufanya naye mahojiano ili kuujua undani wake na kazi yake. [76]
kubaki
Anachoogopa yeye ni kubaki nyumbani akisubiri kuomba badala ya kufanya kazi. [77]
kubwa
Wakizungumza na waandishi wa habari juzi, baadhi ya wananchi hao katika eneo la soko kuu la Arusha, walidai kuwa mgambo hao wakiongozwa na kiongozi wao wamekuwa wakiwasababishia hasara kubwa kutokana na kumwaga bidhaa zao chini. [78]
kufa
Kadri wanavyoathirika wao na sisi pia, na kuporomoka kwa uchumi duniani na hivyo serikali imeanza kuchukua hatua kwa kuunda kamati ya dharura na pia kuhimiza kilimo kwa wananchi ili wasikose chakula na kufa njaa. [79]
kuja
Nikajuta maana katika kuongea hivi, nilikuwa nimewaita wengine wenye mnuko kuja kuongea na mimi. [80]
kukosa
Kutokana na hali hiyo Sitta alisema hakuna haja ya kuwa na mafungu ya vyama vingi visivyokuwa na nguvu, hivyo kusababisha vyama hivyo kukosa sera. [81]
kukutana
Hivyo walipanga muda wa kukutana. [82]
kule
Ndio ndugu, mimi naitwa Kazim ni mwenye mgodi wa madini ya almasi kule Mwadui, tatizo ni kwamba hali kwa sasa imekuwa mbaya mno, nimechanganyikiwa hapa hata sijui la kufanya,” alisema akiomba ushauri. [83]
kumbe
Atakufundisha mambo mabaya na kukufanya uamini ni mwenzie kumbe nia yake ni kukuharibia. [84]
kumuua
Ndio akaona ni bora awapigie simu wale jamaa zake na kuangalia ni namna gani wanaweza kumuua albino ili waendelee na biashara ile ya madini na uvuvi wa samaki. [85]
kuna
Slaa alisema kuwa alitahadharishwa na mtu anayemfahamu kuwa kuna kinasa sauti alichotegeshewa kwenye chumba chake na aliporudi alianza kupekuwa hadi akakikuta kimepachikwa kwenye chaga na alipowaeleza wenzake na kupekuwa wakakuta kingine kwenye chumba cha Dk Ali. [86]
kununua
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amewaonya wanachama wa CCM waliozoea kununua uongozi kuwa, sheria ya sasa iliyopitishwa na Bunge itawabana. [87]
kuongoza
Tunashauri kuwa kutokana na fuindisho hilo, katika kipindi hiki cha uchaguzi wa BFT watajitokeza watu wengi kuomba ridhaa ya kuongoza chama hicho. [88]
kuoza
Lakini alipofika kwenye tenga la tatu akaanza kutupa samaki mmoja baada ya mwingine, maana kila mmoja alionekana kuoza. [89]
kutafakari
Nikajaribu kutafakari. [90]
kutibu
Zaidi ya kuwa msaidizi wake, jamaa huyo albino, alikuwa ni mvumbuzi wa dawa kutibu kansa ya moyo, hata hivyo hakuwahi kumwambia Kazim. [91]
kutoa
Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tenda alipotakiwa kutoa maoni yake alikiri kuwa wapinzani walizidiwa lakini akaelezea kuwa hiyo ni changamoto kwao katika kuhakikisha vinakuwa na wabunge wengi ili waweze kuwa na nguvu ya maamuzi bungeni. [92]
kutunga
Ninaziba masikio na kujifanya sijasikia chochote na ninampa muda mwingine wa kutunga wimbo mwingine lakini sitamjibu kabisa. [93]
kuu
Nimeelezwa kuwa Shinyanga mna tatizo la ukosefu wa soko kuu, umeme unatakiwa Bukombe, lakini nimefarijika kuwa mmejenga maduka 135 mjini hapa na yatakuwa ni kitega uchumi kizuri sana kwenu na mgogoro uliopo kwenye kiwanja cha CCM nimeusikia na suala hilo litafanyiwa kazi," alisema Rais Kikwete. [94]
kuua
Ni suala la kawaida kuua albino na damu zao au viungo vyao tunavitumia kwenye shughuli hizo za uchimbaji madini na uvuvi, watu wengi wanafanya hivyo. [95]
kuuza
Hata hivyo, kutokana na msako huo, wafanyabiashara wa mifuko hiyo walilalamikia Manispaa ya Arusha kwa kukiuka sheria za nchi kwa kuzuia kuuza mifuko ya plastiki iliyoruhusiwa imeidhinishwa na serikali na shirika la viwango nchini (TBS). [96]
kuwaza
Nikaendelea kuwaza huku nikiangalia wachuuzi wale, nikagundua kitu kingine cha ajabu. [97]
kuweza
KUPITISHWA kwa muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2008, kutavikwamisha vyama vya siasa vya upinzani kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja ili kukiondoa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM), imebainika. [98]
kwa
Lakini Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Omar Mganga alisema jana kuwa vifaa hivyo vya kielektroniki vina uwezo wa kurekodi kwa muda wa saa 10, lakini haviwezi kupiga picha. [99]
kwako
Na wanakuja kwako wakiwa wanapeperusha hii bendera ya urafiki. [100]
kweli
Ni kweli, wamo vigogo walio serikalini, hilo siwezi kuficha, mawaziri, wabunge na wengine ni makada wa Chama Cha Mapinduzi, hiyo sifichi wamo," alisema Msolopa. [101]
la
WATAALAMU wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, wamewasili mjini Dodoma na kuthibitisha kuwa vifaa vilivyokutwa kwenye vyumba vya wabunge wawili wa upinzani vina uwezo wa kunasa sauti. [102]
lake
Akizungumza jijini jana Norah alisema kwa sasa ameamua kurudi rasmi katika uwanja wa sanaa, kwani alipumzika kwa kipindi kirefu na lengo lake lilikuwa kwa ajili ya kujifunza mazingira kwanza kwa kupitia wasanii wenzake. [103]
langu
Lengo langu ni kuwa dereva, hivi sasa nakusanya pesa kidogo kidogo ili zinisaidia kusomea udereva hasa wa magari makubwa ya abiria," anasema. [104]
ligi
Hata hivyo, Maximo alisema hawezi kuchagua wachezaji wa Taifa Stars kutoka Zanzibar kwa kuwa ligi ya Zanzibar haina kielelezo kamili cha kumtathmini mchezaji kwa kuwa inachezwa katika kipindi kifupi. [105]
lugha
Pia kina chaguzi mbalimbali za lugha ambazo zinaweza kutumika. [106]
maalum
Sherehe hizo ambazo pia zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM mkoa wa Dar es Salaam na wageni maalum kutoka Chama cha ANC cha Afrika Kusini, ni mfululizo wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama hicho ambazo zinafanyika kitaifa mkoani Shinyanga. [107]
macho
NILIPOMUONA kwa mara ya kwanza, sikuamini macho yangu. [108]
madai
WAKAZI wa Manispaa ya Arusha, wamelalamikia vitendo vya kibabe vya mgambo wa Halmashauri ya Manispaa ya Arusha kuwamwagia chini bidhaa zao ikiwemo mchele na mboga ambazo wamekuwa wakinunua katika masoko kwa madai wakitafuta mifuko ya plastiki. [109]
magari
Amepanga kusomea udereva wa magari makubwa. [110]
magumu
Muswada huu uliopitishwa na bunge unaweka mazingira magumu kwa vyama vya siasa vya upinzani hasa vyenye wabunge na madiwani kuweza kuridhia makubaliano ya kuunda muungano, kwa sababu kufanya hivyo moja kwa moja wapoteze nyadhifa zao. [111]
maiti
Na nikishajibwaga ni kulala kama maiti mtarajiwa hadi asubuhi. [112]
makao
Mwajuma Hassan mkazi wa makao mapya, ambaye alimwagiwa bidhaa zake juzi katika eneo la soko kuu la Arusha, alidai kuwa mgambo hao bila hata kumuuliza walimvamia akitoka sokoni na kumwagia mchele wake chini. [113]
makubwa
Mwinyi pia aliusifu utawala wa awamu ya nne wa Rais Kikwete kuwa umefanya mambo makubwa na hasa kusahihisha makosa ya awamu zilizopita. [114]
mara
Alisema waliozoea uongozi wa kununua sheria hiyo itakuwa ni chungu kwao na kuwataka waanze mara moja kunadi sera zao badala ya kusubiri chama kiwasaidie wakati inajulikana wazi kuwa ni mzigo ambao hauuziki bila kutoa chochote kwa wapiga kura. [115]
matenga
Kandokando yake yalikuwepo matenga ya samaki na mchuuzi alikuwa anayakagua moja moja. [116]
mauaji
Kwenye gazeti moja liliandika kichwa cha habari kikubwa kuwa ”Siri ya mauaji ya albino yafichuka, ni kiungo kimoja kuuzwa milioni 100”...alisoma taarifa hiyo na kusema kama gazeti limeandika hivi bila shaka kuna ukweli dhidi ya madai haya kwamba mtu anaweza kuwa tajiri kwa kutumia viungo vya binadamu. [117]
mbele
Akisoma shitaka hilo, mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo, Angela Ngasoma, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama hiyo, Justin Joseph alisema kuwa Januari 27 mwaka huu, mshitakiwa alikamatwa katika mechi kati ya Yanga na Mtibwa akiwa na tiketi ya kughushi. [118]
mbinu
John Macha alisema, inavyoonekana kuna mbinu ya kuingiza mifuko mingine katika masoko ya Arusha kwa manufaa ya baadhi ya watu kwani haiwezekani nchi nzima mifuko hiyo iliyoidhinishwa na serikali itumike na kupingwa Arusha pekee. [119]
mbunge
Katika majibu yake, Marmo alitumia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 71 kifungu cha kwanza ambacho kinazungumzia juu ya mambo ambayo yanaweza kumfanya mbunge kupoteza madaraka yake. [120]
mdogo
Unasema nini Makengeza? Unaogopa uozo mdogo? Ona minofu ya waliooza. [121]
mema
Atageuza mambo mema kuwa maovu na kuonyesha kosa katika matendo yako mema na huenda anafurahia mabaya yaliyokukuta huku akijifanya kukuhurumia, utaona vile anavyokuzungumza kwa watu. [122]
mfupi
Lakini muda mfupi baadaye usumbufu wa kilevi ulipozidi ndani ya gari, kondakta huyo, alivaa uhusika wake halisi. [123]
mimi
Siamini kwani hivi sasa mimi si Mwasiti yule wa zamani, hii yote ni kutokana na kujituma kwangu sambamba na mafunzo ya nguvu na ushirikiano wa karibu kutoka kikundi cha Tanzania House of Talent (THT)," anasema Mwasiti. [124]
miwili
Naye nahodha wa timu hiyo, Mzee Mayala alisema kuwa kwa sasa wameiva tofauti na ilivyokuwa miaka miwili iliyopita, kwani timu ilikuwa haina uzoefu. [125]
mno
Maelezo haya yanafanana kabisa na matukio ya hivi karibuni ya Rais Jakaya Kikwete alipokuwa katika ziara mkoani Pemba kuwabeza wapinzani na kuwakatisha tamaa kwamba inawezekana ikawachukua muda mrefu mno kuongoza dola au hawataweza kabisa. [126]
mnuko
Au hata akibaki hajaoza, bado atanuka kama wenzie maana amekaa kwenye tenga la mnuko mtupu. [127]
moyoni
Hawezi kuweka kitu moyoni, tena yuko tayari kupoteza urafiki wenu kutumia mdomo wake. [128]
msingi
Anatoa wito kwa wanawake kujishughulisha kwani njia za kujipatia pesa ni nyingi na kwamba jambo la msingi ni kuwa wabunifu. [129]
mumewe
Mkewe Kazim, hajui chochote kuhusu mumewe kuua albino; ni mwanamke ambaye anafanya kazi ofisi ya usalama wa taifa na zaidi ya yote anaijua vizuri sheria. [130]
muziki
Ross kabla hajaingia kwenye muziki alikuwa askari polisi. [131]
mwa
Ikabidi tuuweke uchumi mikononi mwa wananchi. [132]
mzuri
Huu, tunaamini kuwa ni uamuzi mzuri ambao unalenga katika kuzipa nafasi timu zote kujiandaa na mechi za ligi hiyo. [133]
nami
Nilipenda sana kuwa msoni na nifanye kazi za ofisini, lakini sikubahatika kusomeshwa, kwani wazazi wangu hawakuwa na uwezo huo, ilinilazimu nijitose huku walau nami niwe na kipato changu kwa kazi halali," anasema. [134]
nao
Ngoma imefanywa, studio za TAYOa, unaona bwana, mtayarishaji wa ngoma anaitwa Bakunde, huyu jamaa alifanya pia ile ngoma ya Jide iliyojulikana kwa jina la Distance, na video ikachapwa na kalaghe, si unajua siku hizi kalaghe Pictures ilivyotangaza njaa? Na iko mtaani kwa sasa, kila mtu anaifurahia kana kwamba ni kazi ya Jaydee peke yake, na wana machozi wana imani bwana, hata Dada Jide akiwa na kazi zake, anaweza akatuacha na vijana tum tujala nao 'Bata' mbili tatu, na burudani ikawepo kama kawaida. [135]
navigator
MSIE = navigator. [136]
naye
Kwanza alipambana naye mlangoni, lakini mlevi huyo akafanikiwa kuingia kwenye gari na dereva akaanza safari kutoka Kituo cha Relini, Tabata kuelekea Gongolamboto. [137]
ndani
Slaa alipelekewa na mtu ambaye hamfahamu, ikiwa na matobo matatu juu na kuhisiwa kuwa inawezekana ndani ilitiliwa kitu ambacho kinaweza kumdhuru mtu. [138]
ndio
Nangole alisema, makundi yaliyopo ndani ya CCM katika wilaya hiyo ndio ambayo yamekuwa yakichangia CCM kushindwa na CHADEMA jambo ambalo sasa lazima likomeshwe. [139]
ndiye
Jamaa huyo ambaye alikuwa kama msaidizi wake wa karibu, alikuwa akimuwakilisha katika kazi mbalimbali na ndiye aliyekuwa ana siri zake nyingi. [140]
ndiyo
Hizo ndiyo sera nzuri za CCM," alisema. [141]
ndo
Hakuna anayeelewa, uchunguzi ukifanyika ndo tutajua, lakini hana haja ya kuogopa kama mambo yake anayofanya yako kwenye mstari," alisema Kimaro. [142]
ndoto
Mwasiti anasema anawapenda wazazi wake kutokana mapenzi ya dhati wanayomuonyesha ikiwa ni pamoja na kumruhusu kufanya muziki, anasema ndoto zake za baadaye ni kuwa mwanamuziki wa kimataifa sambamba na kuwa balozi akiiwakilisha dunia nzima hasa katika masuala ya kijamii. [143]
ndugu
Alisema, asilimia 80 ya mashauri ya kesi mahakamani zinasikilizwa na mahakimu hivyo ni vyema serikali ikaangalia uwezekano wa kuboresha maslahi yao ili kuwaepusha na vishawishi vya kupokea rushwa kutoka kwa wahusika ama ndugu zao. [144]
ngozi
Ukweli ni kwamba wapo pia katika kundi la marafiki, 'marafiki maadui' waliojivika ngozi ya urafiki. [145]
ni
Vifaa hivyo ni Digital Recoder (vinasa sauti vinavyohesabu kwa tarakimu) aina Edic – Mini Tiny. [146]
nia
Sina nia ya kuhama na siogopi kwani wamenifungua akili na siwezi kukimbia matatizo,” alisema Dk. [147]
nikiwa
Ukiachilia yote hayo kubwa zaidi linalonifanya nijivunie ni wimbo ‘A New Day For Africa' ambao tuliimba wasanii wote wa Afrika kwa kuwa nilitumbukiza vionjo nikiwa na Prof. [148]
nyasi
Wana uwanja wa nyasi bandia na hoteli nzuri za kisasa. [149]
nyingi
Barrick Gold ni kampuni ya Canada ambayo katika nchi nyingi imehusishwa na uharibifu mkubwa wa mazingira,"ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya kamati ya maadili kwenda kwa serikali ya Noryway. [150]
nyuma
Miaka ya nyuma ilikuwa ajabu kuona mwanamke akiwa kondakta wa daladala, wachache walikuwa kwenye mabasi ya masafa-Royal Sumayi, Scandnavia Express, Fresh ya Shamba, Dar Express, Kilimanjaro Express na mengineyo. [151]
nyumba
Nikamlaani mwenye nyumba. [152]
nzuri
Alisema sera ya ujamaa iliyoanzishwa na Mwalimu Nyerere ilikuwa nzuri, lakini kutokana na watendaji kutokuwa waaminifu aliowafanananisha na kunguni, sera hiyo ilikufa. [153]
of
Pitt amechaguliwa kwa kuwa muigizaji bora wa filamu ya The Curious Case of Benjamin Button ambayo aliigiza kama mtu mwenye umri mkubwa kuliko alionao. [154]
pia
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya awali ya polisi, wamebaini pia kuwa, Dk. [155]
pili
Alisema kazi anayoifanya Kikwete kwa sasa ni kurekebisha makosa yaliyofanyika katika awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu. [156]
roho
Nakufa, mkuu wa polisi unaniua, sawa mimi nimemuua albino, lakini wewe unaniua mimi kwa kunipiga kibao, imeandika wapi kwamba muharifu apigwe, kabla ya kufikishwa mahakamani,” alisema Kazim huku akikata roho. [157]
sasa
Mwinyi ambaye kwa siku za karibuni ameanza kuhubiri siasa zisizokuwa na unazi wa kichama kama ilivyo kwa mtangulizi wake Mwalimu Nyerere, alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia katika maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho sasa kimetimiza miaka 32, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mwembeyanga, Temeke jijini Dar es Salaam. [158]
si
Bahati mbaya watu hawa walikopa fedha za serikali, nategemea tuliowataja watachukua hatua ya kulipa madeni yao katika muda tuliowapa, wasiolipa wanakabiliwa na adhabu, hii si mzaha wameichezea nchi," alisema Msolopa. [159]
sio
Alisema wapinzani sio maadui, na kwamba Watanzania walikubali wenyewe mfumo wa vyama vingi, yeye akiwa mwasisi wa mfumo huo, licha ya kwamba asilimia 80 walikuwa wameukataa maoni ya asilimia 20 ya watu waliohojiwa yalikubaliwa. [160]
soka
Shirikisho la Soka Tanzania, TFF liliiomba Yanga kuwaacha wachezaji wa timu hiyo walioko Taifa Stars, lakini uongozi wake ulikataa kwa maelezo kwamba pamopja na ushindi wa mabao 8-1, lolote linaweza kutokea katika soka. [161]
soko
Mwinyi alitumia nafasi hiyo kutakasa sera ya soko huria, maarufu kama ruksa, aliyoanzisha mwenyewe baada ya kuingia madarakani kurithi mikoba ya mwalimu mwaka 1985, akisema kuwa hiyo ilikuwa ni hatua ya kurekebisha hali iliyokuwa taabani. [162]
tajiri
Huku akiendelea na kazi Kazim alikuwa ni mtu tajiri kwa muda mfupi mno. [163]
tena
Mgambo hao, ambao mapema mwaka juzi walilalamikiwa na wananchi kwa Rais Jakaya Kikwete kutokana na vitendo vya unyanyasaji mitaani ikiwepo kunyang'anya bidhaa za watu, juzi wameanza tena zoezi la kukamata watu wanaoonekana wamebeba mifuko hiyo barabarani. [164]
tiketi
Naye Mbunge wa Vunjo kwa tiketi ya CCM, Alloyce Kimaro alisema Dk. [165]
tu
Haya yalikwenda vizuri tu mpaka walipozuka kunguni wakapekecha mfumo," alisema Mwinyi na kuufananisha mfumo wa ujamaa unaodaiwa kuwapo sasa kama mti uliopekechwa na wadudu. [166]
tuzo
Wachezaji hao watatangazwa na kuzawadiwa katika hafla ya kutoa tuzo za mwanasoka bora Afrika zitakazofanyika kwenye mji wa Lagos keshokutwa, sanjari na mkutano mkuu wa CAF. Orodha ya wachezaji hao imependekezwa na makocha 54 wa timu za taifa za mataifa ya Afrika. [167]
uko
Sasa Kazim ujue kwamba uko chini ya ulinzi, kwa sababu ni mgonjwa sana tutakufunga pindu hapa wakati tunaangalia namna ya kukufanyia, uko chini ya ulinzi,” alisema mkuu wa jeshi la polisi ambaye alionekana kusononeka sana kwa kifo cha yule mvumbuzi wa dawa. [168]
ule
Waliopekecha mfumo ule walikwenda mbali na sisi tuliomrithi Baba wa Taifa tukagundua hali hiyo jinsi ilivyokuwa mbaya, kiasi ambacho hata ukitaka sabuni dukani hadi upange foleni. [169]
uozo
Samaki wote wakioza, atabaki wa kuuza? Samaki wakiwa wazimu, mzima atapatikana wapi?'Na hapo nikajikuta nimekaa chini huku harufu ya uozo ikiwa imeniletea kizunguzungu. [170]
ushauri
Tunaamini kuwa hili linawezekana kwa makocha na uongozi wa klabu hizo wakizingatia ushauri huo na kuachana na sababu, kujiandaa vizuri wakati huu wa mapumziko ya Ligi Kuu. [171]
usiku
Siku moja usiku akiwa nyumbani alitafakari sana hali ngumu ya maisha ambayo angeanza kuishi. [172]
utata
Hata hivyo alisema ni bora kusubiri uchunguzi ufanyike na majibu yatakayotoka yatamaliza utata uliopo. [173]
vyake
Machoni alionekana kama mwanamke mwingine yeyote, lakini vitendo vyake vilimfananisha na kondakta mwingine yeyote. [174]
vyao
Ni matumaini yetu kuwa timu hizo zitatumia mapumziko hayo kwa ajili ya kuviweka vizuri vikosi vyao ili kuweza kuupa raha mchezo wa soka. [175]
wakubwa
Wakaanza kunisukumia samaki wakubwa wakubwa wenye harufu isiyovumilika lakini wao walionekana kufurahi tu. [176]
walioko
Yanga itaondoka katikati ya wiki ijayo kwenda Comoro kwa mchezo wa marudiano wakiwemo wachezaji walioko kwenye ya taifa kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika. [177]
waliooza
Ilionekana wazi kwamba waliooza zaidi ni wale wa juu, kisha wale wa juu walikuwa wameambukiza wale wa chini uozo wao. [178]
waliopo
Miongoni mwa maneno hayo ni "Shame! Shame! Shame!..." wakiimanisha "Aibu! Aibu! Aibu!..."Zitto alitaka kipengele hicho kionyesha kinawahusu tu viongozi ndani ya vyama na kisiwaguse wale waliopo kwenye mchakato wa taratibu za kuchaguliwa na wananchi kiserikali. [179]
wamo
Habari ambazo Mwananchi Jumapili inazo zinaonyesha kuwa, miongoni mwa wadaiwa wa mfuko wa CIS wamo mawaziri, wabunge, makada wa CCM na wafanyabiashara wengine maarufu. [180]
wananuka
Na hata wachuuzi wenyewe walikuwa wananuka. [181]
wao
Lakini msimamo wao ulikuwa ni sawa na 'dua la kuku ambalo halimfikii mwewe’ kwani walipokuja juu, Naibu Spika wa Bunge, Anne Makinda aliamua zipigwe kura na wingi wa wabunge wa CCM ukafanya upite kilaini. [182]
watu
Kutokea kwa tukio hilo kumewaacha midomo wazi watu wengi, hasa wakitaka kujua sababu za wabunge hao kuwekewa vifaa hivyo kijasusi ambavyo vinaweza kubaini siri za wabunge hao. [183]
wenu
Anakuwa mwema zaidi anapokuwa na shida, katika kipindi chako cha mafanikio urafiki wenu utanoga, ukifilisika atakugeuka. [184]
wenzao
Kikwete, Karume na Pinda wanachokiamini kinafanana na walichokiamini watumwa wa shimoni ambao waliukataa ukweli na kuendelea kuwapotosha watumwa wenzao. [185]
wetu
Tumsifu kijana wetu Kikwete, amefanya kazi nzuri. [186]
wiki
Ijumaa wiki hii wakati wa kupitishwa muswada huo bungeni, vyama hivyo baada ya kushindwa kuuzuia usipitishwe wabunge wake walibaki wakizomea: "Shame! Shame! Shame!" huku wabunge wa CCM wakishangilia baada ya kuupitisha kwa kura nyingi. [187]
wimbo
RAPA kutoka Miami, Rick Ross amesema hataujibu wimbo wa 50 Cent ambao unamhusu yeye moja kwa moja. [188]
wote
Polisi walieleza kuwa kwa muda wote huo, Dk. [189]
yake
Slaa hajawahi kulalamika polisi juu ya tatizo lolote linalohusu wasiwasi juu ya maisha yake. [190]
yale
Mtazamaji siku zote humkosoa anayecheza, sasa awamu ya nne imetazama makosa yale na inarekebisha. [191]
yalikuwa
Lakini kwa hao mambo yalikuwa kinyume kabisa. [192]
yao
Alifafanua pia baadhi ya kampuni hizo zipo katika mazungumzo na kampuni yake kuhusu utaratibu wa kulipa madeni yao, na kampuni yake itakamata mali za wadaiwa na zisipokidhi madeni yao hatua zaidi zitachukuliwa. [193]
yetu
Katika Kata yetu hii ya Rotya ni mfano kwani sisi kila kijiji kina sekondari na sio Kata tena na hii ni utekelezaji wa vitendo wa Ilani ya uchaguzi ya CCM," alisema Tipe. [194]
yote
Sisi tulikwishakwenda kuonana na Mkurugenzi wa manispaa juu ya mgogoro huu na kimsingi alituelewa kuwa mifuko ambayo inapaswa kupigwa marufuku ni ile isiyo na TBS ambayo inatoka nchi jirani ya Kenya lakini sasa maafisa wake wanapiga marufuku mifuko yote na kuwasumbua wateja," alisema Macha. [195]
za
Vifaa hivyo viligundulika Alhamisi iliyopita vikiwa vimetegeshwa kwenye chaga za vitanda wanavyolalia. [196]
zamani
Amokachi, mchezaji wa zamani wa Super Eagles, alisema nchi hiyo iko katika mazingira mazuri yanayoruhusu timu yake kucheza mechi. [197]
zangu
Naomba nichukue furasa hii kuwasabahi marafiki zangu popote mlipo. [198]
zenye
Katika hatua nyingine Maximo alisema jana kuwa klabu za Simba, Mtibwa Sugar, Yanga na nyingine zenye wachezaji timu ya taifa, hazina budi kumshukuru kwa kuwatengenezea wachezaji wazuri. [199]
ziko
MAHAKAMA Mkoani Kilimanjaro ziko hatarini kufunga huduma za kimahakama katika wilaya mbalimbali za mkoa kutokana na uchakavu wa majengo yanayohatarisha maisha ya binadamu. [200]