Mabano/parandesi/braketi/vifungo.

Mabano ni nomino.

Mabano yako katika ngeli ya ya-.

Mabano ni alama za nusu mviringo zinazotumika kuzingira maandishi. Kwa mfano: (nukta). Kisawe cha mabano ni braketi.

Parandesi ni ( ), / /, { } au [ ].

Matumizi ya mabano. 1. Kufungia maneno yatoayo maelezo zaidi kuhusu maneno yanayotangulia. Mfano: aliootelea jijini (Nairobi). 2. Kubainisha nambari katika orodha. Mfano: (1.)...(2.)... 3. Kubainisha herufi katika orodha. Mfano:(a)...(b)...