Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-02-04

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aaah
Yaani niue albino ndio niwe tajiri, aaah hapana sitaki kuwa kwenye orodha ya wauaji, kama ni umaskini acha niwe, hata kama watu watasema nimeporomoka sawa tu,” alijisemea Kazim. [1]
acha
Kama hii hapa chini We Makengeza, Wewe ni mwanamume au la? Kama ni mwanamume, acha kutoa viliovilio vyako vya kipuuzi kila siku maana naona unaanza kuwaambukiza hata wengine. [2]
aende
Kuna baadhi na wataalam kule alikokwenda kuhangaika walimshauri labda aende nje ya nchi. [3]
agizo
Akiongozwa na mwendesha mashtaka wa serikali, Bwire alisema aliandika barua hiyo kwenda kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuvifanyia uchunguzi vielelezo vya udongo wenye damu kwa agizo la Mkuu wa kitengo cha utambuzi wa vilelezo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Mgawe. [4]
aina
Tukio hilo ni la pili kwa maafisa wa polisi kujeruhiwa mkoani humo, kwani wiki moja kabla ya hapo, Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Olmolong, wilayani Siha, Stesheni Sajini Gaston alijeruhiwa vibaya na mtuhumiwa wa mauji ailiyekuwa anasakwa kwa tangu 1998, ambaye katika mapambano hayo alifanikiwa kupora magazine ya bunduki aina ya Shot Machine Gun (SMG) ikiwa na risasi 29 na kukimbia nayo. [5]
ajabu
Migomo na maandamano ya ajabu ajabu inatukera sana, na hii ni changamoto nyingine kubwa katika kufikia lengo la kuboresha elimu yetu. [6]
akawa
Kweli walifanya hivyo, wiki moja baadaye walirudi, Kazim akawa amekubali kwamba angependa kufanya biashara zote mbili yaani ya uvuvi na uchimbaji madini. [7]
akiwa
Kwa mujibu wa habari hizo, mtoto alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Rulenge wilayani Ngara. [8]
alidakia
Mwishiwa mwingine alidakia. [9]
alitoa
Baada ya wakili Rweyemamu kutoa sababu hizo na kuomba mahakama kumwachia, Jaji Shayo alitoa uamuzi wa kumwachia huru mtoto huyo. [10]
amani
Katika mapendekezi yake pia anaitaka serikali iwachukuwe watoto wote ambao ni maalbino nchini na kuwapeleka katika shule mbalimbali za bweni na iwahakikishie usalama wao kwa kutoa ulinzi ili wasome kwa amani. [11]
ambao
Alisema endapo watuhumiwa watakamatwa, ni wazi kuwa watawataja watu ambao wamewakodisha kwa ajili ya kufanya kazi hiyo. [12]
ambazo
Katika ushahidi wa jana, akihojiwa na Wakili Majura Magafu, shahidi SP Bwire alikiri kupokea sampuli za udongo zilizodaiwa kutoka katika eneo la tukio la Sinza, ambazo zilipekwa kwa Mkemia Mkuu wa serikali ili kuchunguzwa kama zilikuwa na damu za binadamu. [13]
ana
Rweyemamu pia alidai kuwa kijana huyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 17, amesota rumande kwa kipindi kirefu na kwamba, kama mahakama ingekuwa imesikiliza kesi hiyo mapema, ingekuwa tayari imemwachia kwa kuzingatia kuwa alikiri kutenda kosa alipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza. [14]
anaweza
Waziri Mkuu anaweza kujihakikishia hili kwa kupitia kwenye vitengo mbalimbali kufanya uhakiki wa wataalamu, kujua wangapi wanajua nini, na kwa uwezo gani. [15]
angalau
Ndio maana naipongeza serikali ya awamu ya nne ya kutambua umuhimu wa kuongeza kiwango cha elimu ili angalau Watanzania wengi wakahitimu kidato cha nne. [16]
angalia
Hebu angalia kadi za wenyewe. [17]
asasi
Wazazi, asasi na mashirika kadhaa yamekuwa mstari wa mbele kuyasemea haya mara kwa mara. [18]
au
Tunaomba uchunguzwe kujua kama kuna damu na ni damu ya binadamu au damu ya mnyama. [19]
aweze
Katika miaka 10 iliyopita nimeshuhudia ukuaji mkubwa wa matumizi ya teknolojia ya habari, kiasi cha kumfanya Mtanzania aweze kuangalia TV shambani kwake kwa kutumia simu yake ya mkononi. [20]
baiskeli
KAMPUNI ya Simu ya Vodacom imekabidhi baiskeli tatu kwa waendesha Baiskeli watatu kwa ajili ya kushiriki mashindano ya kimataifa ya Baiskeli kwa nchi za Afrika ya Mashariki ambayo yatafanyika Februari nane Nairobi, Kenya. [21]
bali
Hatuwezi kuongozwa na hisia za jazba bali tutaongozwa na sheria na katiba ya nchi” alisisitiza Mohammed. [22]
bara
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, wataalamu hao walisema kuwa Kikwete alifanikiwa kwa kiasi fulani katika masuala kadhaa yanayolikabili bara la Afrika ikiwamo migogoro ya kisiasa na uchumi. [23]
bila
Kufuatia hali hiyo Wakili wake Denis Msafiri aliitaarifu mahakama kuhusu mshtakiwa huyo kutokuwepo kizimbani kulinga na hali yake, lakini akaiomba mahakama iweze kuendelea kusikiliza kesi hiyo hata bila yeye kuwepo kwa kuwa yeye kama mwakilishi wake alikuwepo. [24]
bunge
Fedha hizo zitakuwa nyongeza kwa bajeti ya matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 iliyoidhinishwa na bunge Juni mwaka jana. [25]
chozi
Chukua mfano wa huyu aliyedondosha chozi juzi. [26]
dhidi
Sheikh Ponda alisema, maalbino walioandamana juzi hawakumuelewa Mohammed kwa kuwa, yeye hakupinga vita dhidi ya mauaji, bali alionyesha kosa la kikatiba na kisheria lililofanywa na Waziri Mkuu. [27]
dira
Vijana mnatakiwa kuwa na dira kwa sababu serikali ina dira yake, wizara zina dira zake na mashirika yana dira zao. [28]
es
WAKATI mawakili wa washitakiwa wa kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mhahenge, Morogoro na dereva teksi wa Manzese, jijini Dar es Salaam, wakiwasilisha rasmi hoja za utetedi, mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe amesema hana kesi ya kujibu. [29]
gharama
Hapa kuna utaratibu wa kuchangia gharama kidogo," anasema Mkurugenzi wa shule hiyo Gratho Mbele alipozungumza na Mwananchi hivi karibuni. [30]
haikuwa
Alisema hakubaliana na bao la penalti walilopewa Simba kwani haikuwa la halali. [31]
haina
SERIKALI imesema haina mango wa kulipa madeni yaliyoachwa na vyama vya ushirika katika halmashauri mbalimbali, badala yake inafanya mpango wa kuziwezesha kifedha halmashauri hizo ili ziweze kukabiliana na matatizo yanayozikabili. [32]
hajui
Kauli hiyo ilionekana kumchanganya sana Kazim, akawa hajui la kufanya. [33]
hakuna
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari alisema kuwa Serikali ilishapanga mkakati kuwa halmashauri zinapata ruzuku kutoka Serikalini, hata hivyo hakuna sababu za msingi za kufidia madeni hayo. [34]
hao
Tunatambua kuwa wahalifu wana mbinu nyingi na siye tunapopanga mikakati ya kukabiliana nao, wao pia wanabuni mbinu nyingine, ili wananchi watusaidie kuwadhibiti wauaji hao,” alisema Mwema. [35]
hapa
Mkuu wa jeshi la Polisi nchini,, Said Mwema aliyasema hayo jana wakati akizungumza na askari polisi wa jeshi hilo, maafisa wa polisi na waandishi wa habari jijini hapa. [36]
hapo
Zombe ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, alitoa kauli hiyo jana nje Mahakama Kuu inakosikilizwa kesi hiyo, mbele ya waandishi wa habari na wananchi waliofurika mahakamani hapo jana kusikiliza kesi hiyo, inayogusa jamii. [37]
haraka
Tunaomba majibu haraka,’’ ilisomeka sehemu ya barua hiyo. [38]
hasa
DHANA iliyojengeka akilini mwa watu wengi na hasa viongozi wa serikali kuhusu asasi au mashirika yasiyo ya kiserikali ni kwamba mengi ni ya mfukoni na hayatumii misaada kutoka nje kwa malengo yaliyokusudiwa. [39]
hawa
Inaonesha wenzetu hawa wanatumiwa na wanasiasa,” alidai Sheikh Ponda. [40]
hazina
Inadaiwa baadhi ya asasi hazina hata ofisi wala makao yanayoeleweka na pia inadaiwa zinatumia matatizo ya watoto yatima au wale waishio katika mazingira magumu kujinufaisha. [41]
hicho
Mfaume alisema kiwanja hicho kilichopo kitalu na. [42]
hii
Na hapana shaka ni kwa sababu hii ndio maana waliomba shahidi wa 22 aitwe tena ili kutoa ushahidi kuhusiana na uchunguzi wa vielelezo hivyo vinavyodaiwa kutolewa katika eneo la tukio la Sinza. [43]
hili
Aliongeza kuwa endapo Kikwete angetumia njia ya ushirikishwaji wa wakuu wote wa nchi wanachama wa AU katika utatuzi wa matatizo yanayolikumba bara hili, angekuwa amepiga hatua kubwa zaidi kama mwenyekiti. [44]
hivi
Timu ya watu kutoka makao makuu wakiwemo ofisi ya mkemia, usalama wa taifa, polisi waliobobea kwenye upelelezi, wanasheria wanatarajia kufika jijini hapa kwa ajili ya kuona jinsi ya kukabiliana na vitendo hivi,” alisema. [45]
hizi
Maana, jamani, hizi kadi za biashara ni kama ibada ya dini. [46]
hospitali
Alihangahaika kwenye hospitali nyingi bila mafanikio. [47]
hospitalini
Muda mfupi baadaye waziri alifika hapo hospitalini, kwani si mbali sana kutoka kwenye ofisi yake. [48]
huko
Na kwa bahati mbaya huko ambako tunaagiza maarifa haya, wanazalisha mapya kila siku kiasi kwamba kama hatufanyi warsha na semina tutafika mahali tutapitwa na tutaaachwa mbali. [49]
humo
SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, jana lilituma barua katika klabu ya Yanga ya kuwaombea wachezaji walio katika timu ya taifa kutokwenda Comoro katika mechi yao ya marudiano itakayochezwa Februari 15 nchini humo. [50]
huo
Alisema mkurugenzi huyo aliamua kumtuma Kaimu ofisa mipango wa manispaa hiyo,Mwaisile Lukas kufika eneo hilo ili kujionea ujenzi huo. [51]
hupata
Kituo hicho kina watoto yatima 178 na wajane 72 ambao wote hupata mahitaji ya malazi, mavazi na elimu katika eneo moja. [52]
huru
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba, imemwachia huru mtoto mmoja aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kumuua mtoto mwenzake. [53]
huu
Tunatarajia kukutana hivi karibuni ili tupange mikakati ya chama chetu kwa mwaka huu, lakini pia tunataka kuona idadi ya wachezaji gofu wanawake inaongezeka kwani bado tunaidadi ndogo ya washiriki,"alisema Malaba. [54]
huwa
Wadau hao wamesema kuwa wanafunzi wengi wanaokwenda kwenye shule za binafsi na zile za mashirika ya dini wengi wao huwa hawakuchaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari kwa shule za serikali hivyo hata uwezo wao ni mdogo hali ambayo inawafanya wapate muda wa kuandaliwa kabla ya kujiunga na kidato cha kwanza. [55]
huyo
Alisema baada ya kufuatilia, walikuta mtu huyo ameanza kujenga na ndipo walipoamua kutoa taarifa katika manispaa hiyo na kuamua kuweka pingamizi la kuzuia ujenzi katika kiwanja hicho. [56]
huyu
Kama tuna jamii ya wahitimu wa viwango vile ambavyo mara baada ya kumaliza shule wakatoa talaka kwa vitabu na tabia ya usomaji; na kuwa, kwa mfano, mtu amesoma uchumi, lakini alipoajiriwa benki hajiendelezi tena kusoma, na hatimaye kubakiwa na ujuzi wa kuendesha benki, na kule nyumbani hana hata kamaktaba, ila CD za muziki na sinema tu, sidhani kama mtu huyu hatahitaji tena semina kumkumbusha kuhusu mabadiliko yanayojitokeza katika taaluma yake ya uchumi. [57]
ikiwa
Katika kipindi cha uongozi wake kama mwenyekiti wa Afrika, Kikwete anajiwekea rekodi nzuri ya kuweza kutatua migogoro kadhaa katika nchi za Afrika ikiwa ni pamoja na Kenya, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mafanikio kadhaa ya kutia moyo katika kutafuta suluhu nchini Burundi. [58]
ila
Hata mimi kuna kipindi nilishuhudia mauaji ya kinyama ya vikongwe, lakini si kusema wauaji wauawe, ila tulichofanya ni kuandaa operesheni ya kuwasaka wahalifu na kuwafikisha katika vyombo vya sheria. [59]
ile
Unajua, bara hili lina migogoro mingi sana, kama huna sera zako madhubuti juu ya masuala mbalimbali ni wazi kutakapo tokea shida yoyote ile utafanya mambo kwa haraka haraka tofauti na kama angekuwa na msimamo fulani basi angeweza kusuluhisha kila jambo bila shida. [60]
ina
Alifafanua kuwa, jamii haiwezi kutoa maamuzi kwa hisia kwa kuwa nchi ina miongozo yake na ndio mana alitaka ufafanuzi kwa Waziri Mkuu kuhusu kauli yake, kwa kuwa ilikiuka katiba ya nchi ambayo aliapa kuilinda wakati akikabidhiwa madaraka. [61]
juzi
Baada ya tukio hilo, mtoto huyo alikamatwa na kufunguliwa mashitaka ya mauaji, kesi ambayo ilihitimishwa juzi kwa kijana huyo kuachiwa huru. [62]
kabla
Hivyo basi, kama ombi hili litafikishwa bungeni serikali itakuwa imefuata ushari huo ili matumizi ya fedha yafuate taratibu za kuidhinishwa kabla hazijaanza kutumika. [63]
kadhaa
WASOMI na wataalam wa masuala ya siasa nchini wamesema kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Tanzania kama mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) chini ya Rais Jakaya Kikwete ulikuwa na mafanikio kadhaa. [64]
kansa
Zaidi ya kuwa msaidizi wake, jamaa huyo albino, alikuwa ni mvumbuzi wa dawa kutibu kansa ya moyo, hata hivyo hakuwahi kumwambia Kazim. [65]
kasi
Alisema mikakati itakayosaidia kupunguza msongamano huo ni pamoja na mabasi yaendayo kasi na upanuzi wa barabara muhimu kama vile Sam Nujoma,barabara za Kilwa na Mandela ambazo shughuri zake zinaendelea. [66]
kati
Mahojiano kati ya Wakili Magafu na shahidi SP Bwire yalikuwa kama ifuatavyo. [67]
katiba
KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohammed amesema hata kama watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) wataandamana nchi nzima, hana wasiwasi kwa kuwa hoja yake bungeni juu ya kauli ya Waziri Mkuu kuhusu kuwaua wanaowaua, aliitoa ili kusimamia katiba na sheria za nchi. [68]
kibao
Tunafurahi sana kuona kwamba angalau mmoja wa wale tuliowaona kuwa na roho ya korosho, ambao hawajali mateso ya wananchi ili mradi wanapata posho zao, na marupurupu kibao, na uwezo wa kufisadi wapendavyo, tunafurahi kuona kwamba angalau mmoja wao ameonyesha hali ya kuhuzunika, hata hali ya kushikwa na hasira kutokana na hali hii. [69]
kidato
Kwa mujibu wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995, mhitimu wa elimu ya sekondari ya kawaida (kidato cha IV) mwenye ufaulu wa daraja la III ndiye atachukua mafunzo ya miaka miwili ya ualimu. [70]
kikuu
Msamvu jirani na kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoa mbalimbali. [71]
kila
Alisema katika Mkoa wa Mwanza vitendo vya kuwakata mapanga vikongwe, albino na ajali za barabarani zimekuwa tishio, hivyo jeshi hilo, linafanya kila jitihada za kuhakikisha vitendo hivyo vinadhibitiwa. [72]
kile
GTV imesitisha huduma zake Tanzania na sehemu nyingine duniani kwa kile kilichoelezwa kuwa kukumbwa na mgogoro wa fedha hivyo kampuni hiyo kushindwa kutoa huduma zake. [73]
kilikuwa
Akizungumza kwa njia ya simu, Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Profesa Mwesiga Baregu alisema kuwa kipindi cha uongozi wa Kikwete kilikuwa na mafanikio na pia kilikuwa na mambo kadhaa ambayo hakuweza kuyatekeleza kama kiongozi. [74]
kilimo
Zile zitakazopelekwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika zitagharimia pembejeo za kilimo. [75]
kina
Nyingine ni TPDC, Mbezi (Morogoro road-Malamba mawili-Kinyelezi-Banana, Jet mwisho,Tangi bovu-Goba, Kimara Baruti-Msewe- Changanyikeni na barabara ya Kimara –Kirungule-External  (Mandela) ambazo alisema kuwa zote ziko katika hatua mbalimbali za usanifu wa kina kwa ajili ya kuanza ujenzi. [76]
kinyama
Aliongeza kuwa Pinda si wa kwanza kushuhudia mauaji ya kinyama na wala waliomtanguliwa hawakutoa maamuzi kama hayo ya kukiuka katiba ya nchi. [77]
kisasa
Sumari alisema Serikali kupitia kikao chake cha Baraza la Mawaziri kilichokutana mjini Dodoma Agosti 12, 2005 ilikubali kuanza utekelezaji wa mpango wa mageuzi na uendeshaji wa kisasa wa ushirika nchini na kwamba masuala ya madeni ,yalijifuta tangu wakati huo. [78]
kuahidi
Jax akizungumza mara baada ya kukabidhiwa baiskeli hizo alipongeza Vodacom kwa msaada huo na kuahidi timu hiyo itakwenda Kenya kufanya vizuri. [79]
kubaki
Ni kweli tumetuma barua hiyo leo ( jana) kwa ajili ya kuwaombea wachezaji hao waendelee kubaki kambini kwa ajili ya maandalizi ya ( CHAN) na tumefanya hivyo kwa kuwa tumeona mafanikio makubwa katika mechi yao ya kwanza kwa kuwa wameshinda mabao mengi na kujiweka katika nafasi nzuri. [80]
kucheza
Timu tatu kati ya timu tisa zitakazoshiriki michuano hiyo ya ligi daraja la kwanza zitapanda daraja na kucheza Ligi Kuu ya Tanzania Bara. [81]
kudai
Unajua watu wengi wanajua haki zao lakini wanashindwa kujua njia za kuzipata na hivyo kuamua kutumia vurugu kudai haki hizo," anafafanua. [82]
kufa
Wakati wanaendelea kuangalia ile picha aliingia daktari aliyekuwa akimwangalia Kazim na kumwomba waziri afupishe mazungumzo, badala yake wamsake yule mvumbuzi wa dawa kwani isingepita saa 12 kabla ya Kazim kufa ikiwa hatapata ile dawa. [83]
kufundishia
Sababu kubwa ni kuwa kule kwenye taasisi zetu hakuna vifaa vya kufundishia, wala wataalamu na muda wa kutosha wa kuweza kujifundisha mambo haya. [84]
kuishi
Siku moja usiku akiwa nyumbani alitafakari sana hali ngumu ya maisha ambayo angeanza kuishi. [85]
kujiunga
Lakini inasikitisha kuona hata baada ya kupunguza masharti ya kujiunga na ualimu kuna mbumbumbu na matapeli wa elimu wanaotumia sifa za wengine kuwa walimu. [86]
kule
Je, wataalamu wetu kule shuleni wanakwenda sambamba, katika mafunzo yao, na mabadiliko haya katika masoko ya bidhaa ya TEHAMA? Ninachosema hapa ni kuwa kama nchi yetu, kama zilivyo nchi nyingi za dunia ya tatu, haitajiingiza katika uzalishaji wa maarifa na elimu kwa matumizi ya wananchi wake, na kuwa taasisi za elimu vikawa vitovu vya maarifa mapya ili wahitimu wetu watoke wakiwa sio tu washika vyeti, bali wazalishaji elimu na maarifa mapya, huenda tunaweza kupunguza utegemezi wa nje na kupunguza mahitaji ya warsha kwa ajili ya wataalamu wetu. [87]
kumbe
Maelezo haya ya askari huyu, yalinishangaza, sikutegemea kusikia kwamba kumbe mauaji haya yanaendelea kuwepo kutokana na uzembe wa watendaji wetu kusimamia majukumu yao. [88]
kupanda
Katika hatua nyingine mshitakiwa wa kesi wa 11 katika kesi hiyo Rashid Lema hakuweza kupanda kizimbani kwa kuwa ni mgonjwa. [89]
kusoma
Alisema hatua hiyo itawasaidia wazazi wao kupata amani na muda wa kufanya kazi badala ya kuwalinda na wao pia watapata muda wa kusoma kwa amani na hatimaye kufaulu vizuri kama watoto wengine. [90]
kuu
Vituko vilitawala kwenye lango kuu huku viongozi wa Simba wakuzia magari yote kuingia kwenye geti hilo kwa madai kuwa walikuwa nafanya mambo yao na kusababisha usumbufu kwa mashabiki waliofikia uwanjani hapo na magari. [91]
kuua
Ni suala la kawaida kuua albino na damu zao au viungo vyao tunavitumia kwenye shughuli hizo za uchimbaji madini na uvuvi, watu wengi wanafanya hivyo. [92]
kwanini
Kama walikuwa wanajua wamefilisika, kwanini walichukua fedha zetu. [93]
la
Alisema CCM ilikuwa ikikilipia tangu mwaka 1994 hadi mwaka 2008, walipopata taarifa kuwa kiwanja hicho kimeuzwa kwa mtu mwingine aliyetambulika kwa jina la Hassan Said. [94]
labda
Baba alikuwa na wasiwasi kwamba labda mwanaye angemdharau lakini mimi nilimcheka. [95]
lake
NIANZE kwa kusema kuwa mimi naungana na Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda kuhusu katazo lake la warsha, semina, kongamano, mafunzo, semina elekezi na majina mengine mengi yenye kusudio moja kama lengo lake ni kudhibiti matumizi yasiyo ya faida ya fedha za wavuja jasho. [96]
lao
Kwa ujumla hali hiyo inatafsiriwa kuwa huenda nguvu ya polisi katika kukabiliana na wahalifu imeshuka au wahalifu sasa wamepata mbinu na nguvu mpya na lengo lao ni kudhoofisha jeshi la polisi ili waendelee kutishia maisha ya raia wapendavyo. [97]
lenye
Aidha alisema, akiwa bungeni mjini Dodoma ameandika mchanganuo/azimio ambalo anatarajia kuliwasilisha kwa Spika Samuel Sitta jana jioni, lenye mambo manne makubwa ya kuboresha mkakati na juhudi ya kudhibiti mauaji yao. [98]
leo
Kesi hiyo iliahirishwa hadi leo itakapoendelea tana mahakamani hapo ambapo upande wa utetezi utatoa hoja zao. [99]
licha
Baiskeli hizo zenye thamani ya zaidi ya milioni 1.8 ni washindi wa mashindano ya Mwanza Cycle Challenge 2008 ambao ni Hamis Hussein, Manga Ezekiel na Richard Laizer na licha ya kupewa baiskeli hizo pia Vodacom inadhamini kambi yao mjini hapa. [100]
ligi
Katibu mkuu wa Mwanza United, Everist Agila alisema kuwa usimamizi mzuri wa TFF ndio utakao saidia kupatikana kwa timu tatu bora zitakazo panda daraja bila ya kuwa na utata kama zilivyokuwa ligi zilizopita. [101]
lini
Alikuwa akijibu swali la Charles Keenja (Ubungo CCM) aliyetaka kujua ni nini kinasababisha kero ya msongamano wa magari katika barabara ya Ubungo na nini ufumbuzi wa jambo hili na lini. [102]
lugha
Mafunzo hayo yalilenga kuwapa stadi wanafunzi hao wayazoee mazingira na lugha ya kufundishia kabla ya kuanza mafunzo kamili ambayo masomo yote isipokuwa Kiswahili na mawasiliano ya kila siku ni kwa Kiingereza. [103]
maeneo
Alisema kazi ya awali, ikiwemo michoro tayari imekwishanza sambamba na kuwekwa kwa alama katika maeneo husika. [104]
mafupi
Baada ya mahojiano hayo mafupi Wakili Magafu alimtaka shahdi huyokuisoma barua hiyo. [105]
magumu
Maximo alisema kuwa mashindano hayo yatakuwa magumu sana kwa sababu kwani kunatimu ambazo zinajulikana katika ulimwengu wa soka kama Senegal na Ivory Coast. [106]
maiti
Baba mmoja akaniambia mtoto wake akamshtukiza akilia mbele ya luninga kwa kuona maelfu ya maiti yaliyorundikana. [107]
mapya
Tunapozungumia ongezeko la warsha, semina na kadhalika tujiulize kama mfumo wetu wa elimu una uwezo wa kuzalisha maarifa mapya. [108]
masomo
Mafanikio makubwa yaliyopatikana hadi sasa ni vijana hao kuwa na uhakika wa kusoma muda wote bila kukatishwa masomo kutokana na sababu yoyote ile. [109]
mauaji
Alisema fedha hizo, zimetengwa kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watu watakaotoa taarifa za uhalifu hususan za mauaji ya albino na vikongwe yanayoendelea kutokea nchini. [110]
mawaziri
Lakini kwa nini tatizo hili la mauaji ya albino kuuawa limeshindikana kudhibitiwa? Mimi nadhani watendaji wa serikali kwa maana ya mawaziri, ndio wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kudhibiti mauaji haya. [111]
mazuri
Alisema tayari walishakaa na uongozi wa Yanga kwa maongezi ya awali kuzungumzia suala hilo na maongezi yalionekana kuwa mazuri kidogo ndio maana wameamua kuwaandikia barua rasmi kuhusu suala hilo. [112]
mdogo
Pia huficha ukweli kuwa uwezo wa walimu wengi ni mdogo na hufanya kazi katika mazingira magumu. [113]
miezi
Anasema kuwa serikali imetoa mwongozo wa miezi mitatu ya mwanzo pindi wanafunzi wanapojiunga na kidato cha kwanza kufundishwa kozi ya Kiingireza hivyo kama shule hizo zitatumia nafasi hiyo vizuri basi muda huo utasaidia kuwaandaa wanafunzi hao kufahamu lugha hiyo badala ya kutumia mwaka mzima kwa ajili ya mafunzo ya awali. [114]
migomo
Mdoe aliwashukia wanafunzi wanaoabudu migomo na maandamano ya mara kwa mara akiitaja kuwa ni miongoni mwa mambo yanayokwamisha dhamira iliyopo ya kuboresha hali ya elimu kwa vijana nchini. [115]
mimi
Nadhani ndugu zangu hawakunielewa na wala hawakuelewa nini taifa linasema, kwa hiyo hata waandamane usiku na mchana nchi nzima mimi sina wasiwasi kwa kuwa nasimamia katiba na sheria,” alisema Mohammed. [116]
minne
Baadaye utaratibu huo ulibadilika mafunzo yakawa yanatolewa kwa kipindi cha mwaka mzima kabla ya mwanafunzi kuanza rasmi kuhesabu miaka minne ya kuwa sekondari kwa ajili ya kidato cha kwanza hadi cha nne. [117]
mkononi
Wakili huyo alisema sababu nyingine ambayo mahakama inapaswa kuzingatia, ni mtoto huyo kutokuwa na kitu chochote mkononi, wakati akimpiga mtoto mwenzake. [118]
mkubwa
Nao washindi hao walipongeza Vodacom kwa msaada huo na kuahidi watarejea nchini na ushindi mkubwa. [119]
mno
Kazi aliaribu kabisa pambano lile na kuwachanganya wachezaji wangu wakashindwa kucheza kwa kiwango chao, maana alitoa kadi nyingi mno akisema faulo, lakini zinapotokea golini kwa Simba hakupiga filimbi za kuonyesha faulo," alisema Kilinda. [120]
mrefu
NDOTO ya Mtanzania, Respicius Baitwa, wa mjini Moshi kwenda kupanda mlima Aconcagua wa Argentina ambao ni mrefu kuliko yote Amerika Kusini imeyeyuka baada ya kuzuiwa Uwanja wa ndege nchini Kenya. [121]
msaidizi
Jamaa huyo ambaye alikuwa kama msaidizi wake wa karibu, alikuwa akimuwakilisha katika kazi mbalimbali na ndiye aliyekuwa ana siri zake nyingi. [122]
muda
Kauli hiyo ya Zombe ilikuja muda mfupi baada ya shahidi wa 22 (PW 22) katika kesi hiyo, Mrakibu wa Polisi (SP), Juma Bwire, ambaye ni Mtaalamu wa Uchunguzi wa silaha na milipuko kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, kumaliza kutoa ushahidi wake kwa mara ya pili. [123]
mumewe
Mkewe Kazim, hajui chochote kuhusu mumewe kuua albino; ni mwanamke ambaye anafanya kazi ofisi ya usalama wa taifa na zaidi ya yote anaijua vizuri sheria. [124]
mwa
Kuhusu masuala ya uchumi, mtaalamu wa uchumi kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dk Haji Semboja alisema Kikwete alijitahidi kwa kadiri alivyoweza kutumia vyombo vya AU, kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc) kuhakikisha kuwa anafuatilia kwa karibu kila hatua ya mabadiliko ya uchumi yanayotkea duniani. [125]
mwamuzi
KOCHA Mkuu wa JKT Ruvu, Charles Kilinda amesema, mwamuzi Othman Kazi, hakuchezesha kwa kiwango kinachotakiwa mechi ya Jkt Ruvu na Simba na alidhamiria kuwatafutia Simba goli kwa muda mrefu. [126]
mwenye
Alisema tofauti na Kikwete, Gadaf anaonekana ni mtu mwenye msimamo na ambaye ana agenda yake juu ya bara hili tangu zamani. [127]
mwezi
Kwa matokeo hayo Simba imebaki kwenye nafasi ya pili na pointi zake 24 huku Yanga akiwa kileleni na pointi zake 39 wakati ligi inapoingia kwenye mapumziko leo hadi Marchi 14 kupisha maandalizi ya Taifa Stars kwaajili fainali za mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) yatakayoanza kutimu vumbi baadaye mwezi huu. [128]
mzazi
Watoto yatima yaani wasio na baba na mama na waishio katika mazingira magumu hulipiwa gharama zote na asasi hiyo wakati wale wenye mzazi mmoja hupata punguzo. [129]
na
HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro huenda ikaingia katika mgogoro na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Morogoro Vijijini, baada ya Manispaa hiyo, kuuza kiwanja cha CCM, hali ambayo imeanza kuleta mvutano baina ya pande hizo mbili. [130]
nadhani
Imekuwa vizuri mechi zote za ligi hii kuchezwa Dar es Salaam, hivyo nadhani TFF itakuwa makini zaidi kuhakikisha mambo yote yanakwenda sawa,"alisema Agila. [131]
naye
Kitenga, mtu mwenye umri wa makamo na umbile la kawaida sana tu, mcheshi usoni na mkarimu moyoni kabla na hata baada ya kujitumbukiza katika ujambazi jina lake lilijulikana kwa wachache hususani kwa sisi tuliyesoma naye darasa moja katika shule ya msingi Mwembesongo mwaka 1976 na kuhitimu 1982, hata hivyo wengi wa wanafunzi hao ambao sasa ni watu wazima walishamsahau na hiyo ilitokana na Kitenga kuacha shule akiwa darasa la kwanza tu na kuingia mitaani kujitafutia riziki. [132]
ndani
Katika hukumu hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba, Augustine Shayo, alimwachia huru mtoto huyo kwa masharti ya kutotenda kosa lolote, ndani ya kipindi cha mwaka mmoja. [133]
ndugu
Katika kesi hiyo, Zombe na wenzake wanatuhumiwa kuwaua kwa makusudi wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Wilaya ya Mahenge, mkoani Morogoro ambao ni Sabinus Sabinus Chigumbi maarufu kama Jongo na ndugu yake Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe Juma Ndugu, dereva teksiManzese jijini Dar es Salaam. [134]
ngapi
Wanaonibisha, waniambie wameangalia kweli kadi ngapi katika hizo alizopewa katika miezi sita iliyopita. [135]
ngozi
JESHI la Polisi nchini, limetenga Sh20milioni kwa ajili ya kuwazawadia watu watakaotoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa wauaji wa vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). [136]
ni
Naye mmiliki huyo Hassan Saidi alisema kuwa, anamiliki kihalali kiwanja hicho ikiwemo kupata kibali cha ujenzi kutoka katika manispaa hiyo na kama kuna makosa yaliyofanyika juu ya kiwanja hicho wakulaumiwa ni manispaa na si yeye. [137]
niwe
Lakini wangapi wameonyesha nia ya kwenda kuona hawa wahanga wenyewe na kutafuta usuluhisho? Nakumbuka msemo mmoja wa hayati Trevor Huddleston aliyekuwa mstari wa mbele kupinga ubaguzi wa rangi 'bora niwe na damu mkononi kuliko maji kama Pilato'.’ 'Una maana gani?' 'Namaanisha hivyo. [138]
ombi
Shahidi SP Bwire alilazimika kuitwa tena mahakamani hapo jana, kutoa ushahidi kwa mara ya pili, kufuatia ombi la mawakili wa watuhumiwa, kwa madai kuwa kulikuwa na utata katika ushahidi uliotolewa na shahidi huyo kuhusu sampuli za udongo wenye damu uliopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi. [139]
one
HALIKUWA jambo la ajabu kukuta baadhi ya shule za sekondari za binafsi na za dini zikitoa mafunzo ya awali ya sekondari kwa wanafunzi wake maarufu kwa Kiingereza kama Pre form one. [140]
pale
Ninafundisha pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kozi ambazo mwanafunzi anatakiwa kujua kupiga picha za video, kuhariri habari au picha kwa ajili ya televisheni au redio; kuchanganya rangi kwa ajili ya maigizo ya jukwaani, sinema au televisheni, aweze kupiga picha za analogi na za "digital", waweze kutengeneza sinema au vipindi vya redio, au waweze kutengeneza kurasa za tovuti na kusanifu kurasa za magazeti. [141]
pili
Lucas alikiri kuwepo na mapungufu katika kutoa umiliki wa kiwanja hicho kwa watu wawili na kwamba halmashauri hiyo, inatambua kuwa CCM ndiye mmiliki halali wa kiwanja,kwani mmiliki wa pili ameanza kumiliki mwaka jana. [142]
raia
Matukio yanaonyesha jinsi vibaka walivyo na ujasiri wa kupamba askari polisi hadi kufikia hatua ya kuwavamia na kuwajeruhi makamanda jeshi hilo lenye dhamana ya kulinda amani kwa raia. [143]
rais
Hata hivyo pamoja na hayo, Profesa Baregu alisema katika kipindi hicho, rais Kikwete hakuwa na agenda moja kwa bara la Afrika jambo ambalo limefanya kuwa na maamuzi ya zima moto kila kunapotokea tatizo. [144]
roho
Wanaume wa kweli tutamwelewaje? Narudia kusema, mwanasiasa anapaswa kuwa na roho ngumu kama jabali ya Mwanza. [145]
saa
Barua hiyo ilieleza kuwa mnano Januari 14 mwaka 2006 saa 12.30 jioni yalitokea mauaji ya watu wanne waliodhaniwa kuwa ni majambazi na kwamba, katika eneo la tukio umechukuliwa sampuli ya udongo wenye damua. [146]
sampo
Mawakili hao walidai kuwa walikuwa na taarifa ya uchunguzi iliyoonesha kuwa sampo za udongo wenye damu zilizopelekwa kwa Mkemia Mkuu zilitoka kwenye eneo la tukio la Sinza, lakini shahidi huyo wa 22 hakuitolea ushahidi. [147]
sawa
Mtoto huyo ambaye wakati tukio hilo linatokea alikuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Rulenge wilayani Ngara, alikuwa anakabiliwa na kesi ya kumuua mtoto mwenzake ambaye kwa umri alikuwa sawa na yeye. [148]
sekta
Waziri Mkuu wa Bunge hilo lililoshirikisha vijana kutoka vyuo na shule mbalimbali za Dar es Salaam, Christopher Mdoe anasema, kuingia kwa siasa katika sekta ya elimu kumechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa ubora wa elimu nchini na akaiomba serikali na wanasiasa kuacha mchezo wa kuingiza siasa shuleni. [149]
shida
Baada ya kesi kuahirishwa Lema aliotolewa mahabusu na kutembea kwa shida huku akiwa ameshikiliwa na washtakiwa wenzake wawili hadi ndani ya gari tayari kwa safari ya kurejea mahabusu katika Gereza la Keko. [150]
sifa
BARAZA la Mitihani la Taifa (Necta), tangu mwaka jana lilianzisha kampeni kamambe za kuwabaini na kuwachukulia hatua wanafunzi wote wanaotumia sifa au vyeti vya watu wengine kupata elimu au taaluma. [151]
sio
Alikunwa na vijana hao kwa kuonesha kivitendo dira waliyonayo kwa kujikusanya kupitia Bunge Kivuli la Vijana ambalo linawapa njia ya kujiandaa kuja kuwa viongozi wa kuzitumikia jamii zao sio kwa cheo tu bali kwa kazi. [152]
sisi
Hata hivyo, sisi hatuamini kwamba, jeshi la polisi limezidiwa nguvu na wahalifu hao, kwani baada ya tukio la kumjeruhi OCD Majjid walifanya msako mkali na kufanikiwa kwakamata vijana ambao mmoja wao alikutwa na saa yake. [153]
siyo
Serikali itambue kuwa mpango wa mafunzo ya awali ya sekondari ulilenga kuwaandaa wanafunzi wanaotoka shule za msingi ambazo Kiingereza siyo lugha ya mawasiliano na hii inazingatia kuwa lugha hiyo ndiyo inayotumika sekondari kwa masomo yote isipokuwa Kiswahili," anasisitiza. [154]
somo
Pia shule ina kompyuta 30 kwa ajili ya kufundisha somo la teknolojia ya habari na mawasiliano. [155]
tabia
Awali akifungua Bunge hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Kamishna Mkuu wa Wizara ya Elimu, Charles Philemon aliwaeleza vijana kuwa ili jamii iweze kupata viongozi mahiri, wenye maarifa na waliokomaa ni lazima vijana wajenge tabia ya kujisomea kwa lengo la kujenga uwezo wa kupambanua mambo. [156]
tajiri
Huku akiendelea na kazi Kazim alikuwa ni mtu tajiri kwa muda mfupi mno. [157]
tatu
Kuachiwa kwake huru, kulikuja baada ya wakili wake, Joseph Rweyemamu, kuiomba mahakama imwachie kwa kuzingatia sababu tatu. [158]
tu
Ikiwa kauli ya Pinda ingefanya kazi kwa kumuua aliyetuhumiwa kumua albino ni wangapi wangeuawa? Je, sheria ndivyo inavyotaka? Au ukiwekewa kidole cha albino nyumbani mwako, halafu ukauliwa, huyo aliyekuua ana uhakika gani kuwa na yeye siku moja hatauliwa na ndugu zako? Kwa hiyo tungetengeneza msururu wa mauaji kwa jazba tu,” alisema Mohammed. [159]
ujumla
Alisema kampuni hiyo imewadhamini waendesha baiskeli hao kama sehemu ya mchango wake katika maendeleo ya michezo na jamii kwa ujumla wake. [160]
uko
Sasa Kazim ujue kwamba uko chini ya ulinzi, kwa sababu ni mgonjwa sana tutakufunga pindu hapa wakati tunaangalia namna ya kukufanyia, uko chini ya ulinzi,” alisema mkuu wa jeshi la polisi ambaye alionekana kusononeka sana kwa kifo cha yule mvumbuzi wa dawa. [161]
una
Alidai Bageni alimsifia kwa kuweza kuona damu hiyo wakati wengine waliowahi kufika hapo na hawakuwa wameiona na ndipo wakachukua sampuli za udongo huo ili ukafanyiwe uchunguzi na mkemia mkuu wa seriali kujua kama una damu ya binadamu au ya mnyama. [162]
uso
Wasichana wangapi wamelazimika kukutana na nduli Ukimwi uso kwa uso kwa sababu baba zao na mama zao wamekosa kazi kutokana na hali ya uchumi iliyosababishwa na walaji wakuu? Nyumba ngapi zimevunjwa kutokana na hilo? Maisha ya Watanzania mamilioni kwa mamilioni yametishwa na kuharibiwa na vitendo vya ukatili. [163]
utafiti
Alisema Kanda ya Tanzania ina wanachama 22, ambao ni Bodi ya kahawa Tanzania (TCB), Kituo cha utafiti wa zao la kahawa (TACRI), Tanzania Coffee Curing, Chama kikuu cha Ushirika cha mkoa wa Kilimanjaro (KNCU), na Chama cha ushirika cha Kagera Coperative Union. [164]
utoro
Mikakati mingine ya wilaya ni kudhibiti utoro wa wanafunzi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanafika na kuingia darasani na pia kuhakikisha wanaoandikishwa darasa la kwanza wanamaliza darasa la saba. [165]
uwanja
Mtanzania huyo ambaye ameshapanda mlima Kilimanjaro mara 80 na mlima Elbrus katika bara la Ulaya, alizuiwa katika uwanja wa Jomo Kenyata nchini Kenya Alhamisi iliyopita na maofisa wa uwanja huo. [166]
vema
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Musa Hassani Mgosi alitumia vema nafasi hiyo kwa kufunga bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 65 ya mchezo. [167]
vifaa
Hukimbilia dawa hiyo kama njia ya kuficha udhaifu wa serikali yenyewe kushawishi ujenzi wa shule nyingi bila walimu wa kutosha na vifaa. [168]
vipi
Huku sasa ni kuzinguana, kumbe hata mawaziri nao huwa wanakuwa wasanii, inawezekanaje niwasiliane na wewe nikiwa nje ya nchi uniambia yuko mvumbuzi wa dawa ya kuponya tatizo langu halafu sasa aniambie hajui atampata vipi, huu ni uhuni,” alijisemea Kazim akiwa mwenye hasira na kuwaza kuwa kama asingempa dawa hiyo angefanya mpango wa kumuua kwa sababu naye alikuwa albino. [169]
vita
Kuhusu nini alichofanya katika vita ya mauaji ya albino kama alivyoulizwa katika mabango ya waandamanaji hao, Mohammed alisema chama chake cha Wananchi (CUF) kiliandaa maandamano makubwa mwaka jana kupinga na kulaani mauaji ya albino nchini. [170]
vitabu
Pamoja na uchanga huo shule imekamilika kwa maana kuna maabara kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi bila matatizo na kuna maktaba inayotoa fursa wanafunzi kusoma vitabu vya ziada. [171]
vituo
Mbele anatoa ushauri kwa serikali iangalie uwezekano wa kuvipatia ruzuku vituo ambavyo vinashughulikia kuwasomesha watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu hapa nchini ili watoto wengi zaidi wasikose haki hiyo ya msingi maishani. [172]
vizuri
Alisema baada ya azimio hilo kuwasilisha kwa Spika, litafikishwa kwa wabunge kwa ajili ya kujadiliwa kama litapita itakuwa vizuri. [173]
vumbi
Ligi hiyo inatarajia kuanza kutimua vumbi hivi karibuni baada ya kusimama kwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara ambapo michezo yote itakuwa ikipigwa jiji Dar es Salaam. [174]
vya
Alisema lengo la kutoa fedha hizo,  ni kuhakikisha vitendo vya mauaji ya vikongwe na albino, vinatokomezwa nchini. [175]
vyake
Kweli wale watu walimuua yule albino na kwenda na viungo vyake kwenye maeneo ya biashara. [176]
vyao
Alisema mpango huo, utafanikiwa endapo polisi watapata taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa watu wanaopewa kazi ya kuwakata mapanga albino, ili kuchukua viungo vyao kutokana na imani za kishirikina. [177]
wa
Hata hivyo, mwenyekiti huyo alisema pamoja na kuweka pingamizi hilo, ameshangazwa kuona mvamizi huyo akiendelea na ujenzi katika kiwanja hicho hali iliyolazimu kuamua kumjulisha Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Raphael Ndunguru ili kujua hatima ya kiwanja hicho. [178]
wajibu
Ndiyo maana wakitumia mwavuli wa Bunge Kivuli la Vijana ambalo lilifanyika hivi karibuni Dar es Salaam wanafunzi nao walijadili nafasi, wajibu na fursa ya kila kijana kushiriki katika uboreshwaji wa elimu nchini. [179]
wakiwa
Tukio hilo lilitokea Oktoba mwaka 2005 wakati watoto hao walipozozana wakiwa katika mchezo. [180]
wala
Hata hivyo shahidi Bwire alipoulizwa iwapo aliweza kupata majibu ya uchunguzi wa sampo hizo alisema hakuwahi kuyaona wala kuisoma taarifa ya matokeo ya uchunguzi huo kwa kuwa yalipelekwa moja kwa moja kwa kiongozi husika. [181]
wale
Hii ina maana kwamba walimu hao 14 na hata wale 800 walikosa sifa hiyo badala yake wakaamua kutumia vyeti vya wenzao walioko kazini au shule nyingine au waliofariki. [182]
wapi
Mwananchi ilishuhudia kundi la wateja wakiwa hawajui waende wapi huku wengine wakiwa wamekata tamaa na kubaki kwenye magari yao wasijue la kufanya, huku wengi wanadai wamelipia na kukatishiwa huduma ghafla. [183]
wasio
Pili inawahudumia wajane na tatu imejenga Shule ya Sekondari ya Tushikamane kwa ajili ya watoto inaowalea na wengine wasio yatima. [184]
waweze
Aidha, Mkurugenzi huyo alitoa wito kwa wananchi wa Tanzania kuzalisha kahawa bora ili waweze kuhimili ushindani katika soko la dunia. [185]
wewe
Je, wewe kijana wa Tanzania una dira gani? Na unatumia juhudi gani ili kufikia dira hiyo?" alihoji na kuongeza kuwa serikali inatambua umuhimu na mchango wa vijana katika nchi kwa kuwapa nafasi ya kujadili na kuhoji mambo yanayoendelea ndani na nje ya nchi. [186]
wiki
JANA gazeti hili lichapisha habari kuhusu Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Moshi (OCD), mkoani Kilimanjaro, Kibawana Majjid kuvamiwa na kujeruhiwa vibaya na vibaka alipokuwa akikagua ulinzi wa doria saa 3.00 wiki iliyopita. [187]
wote
Watoto hao wote walikuwa na umri wa miaka 14 na marehemu alikuwa anasoma darasa la nne, katika shule hiyo hiyo. [188]
yana
Wakati huohuo Katibu Mkuu wa kutetea haki za Waislaam nchini Sheikh Ponda Issa Ponda alidai maandamano yanayofanyika sasa yana mkono na nguvu ya wanasiasa. [189]
yangu
Tiketi yangu ya ndege ilikuwa inapitia London, Unigereza, Miami, Marekani, Santiago, Chile hadi Mendoza Argentina na nilikuwa na Viza ya Argentina nikijua Marekani na Uingereza nilikuwa napita tuîalidai. [190]
yenye
Mkutano huo umeandaliwa na sekretarieti ya EAFCA yenye makao yake makuu Kampala nchini Uganda, kwa kushiriana na wanachama wake. [191]
yetu
Dai lao kuu, kama ilivyo kwa wazazi na wadau wa elimu nchini ni kwamba mfumo wa elimu yetu una upungufu mkubwa kuanzia ngazi ya utungaji sera, mitaala inayotumika hadi usimamizi kisekta. [192]
yuko
Huyu yuko kwenye upande wa madini. [193]
za
Akizungumzia suala hilo ofisa mipango wa manispaa hiyo, alisema manispaa yake ilishaweka pingamizi hilo mapema  katika hatua za awali na kwamba, kwa sasa wapo katika majadiliano kuona jinsi gani ya kutatua mgogoro huo. [194]
zaidi
Aliieleza zaidi mahakama kuwa mara ya pili alikwenda hapo akiwa na mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo SP, Christopher Bageni na kwamba, wakati huo aliweza kuona matundu sita ukutani pamoja na damu kwenye mchanga. [195]
zake
Jitihada zake zilikuwa kubwa na kwa kweli tumeona jinsi alivyofanikiwa kutatua baadhi ya migogoro kwa kushiriki moja kwa moja kama mwenyekiti, mfano mzuri ni mgogoro ulioikumba nchi ya Kenya,” alisema Profesa Baregu. [196]
zetu
Pia tunashirikiana na mashirika, serikali na hata watu mbalimbali binafsi kulaani na kupinga mauaji ya ndugu zetu hao,” alifahamisha. [197]
ziada
Mmoja wa wateja hao alitaka kuingia ndani kinguvu, lakini mlinzi huyo ilibidi afanya kazi ya ziada kumwondoa na kubakia kuzozana. [198]
ziko
Kesi nyingi za mauaji haya ziko mahakamani zinasuasua haziendi kwa madai kuwa ushahidi haujakamilika. [199]
zote
Mengine ni kwa Jaji Mkuu Agostino Ramadhan kuunda Mahakama maalum itakayoshughulikia kesi zote za mauaji ya kikatili kwa albino na vikongwe kwa haraka na ufanisi mzuri. [200]