Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-01-18 : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
d words from Mwananchi Dar es Salaam
 
(Hakuna tofauti)

Toleo la sasa la 22:27, 18 Januari 2009

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aheri
Lakini aheri hata siasa. [1]
akiwa
Habari zilizopatikana ndani ya serikali zinaeleza kuwa katika kujiandaa na uchaguzi mkuu ujao, Kikwete ameamua kuingia katika uchaguzi ujao akiwa na timu mpya ya watu wasafi ambao hawataipa shida CCM kujinadi kwa wapiga kura. [2]
alikuwa
Kuona hivyo mgombea wa chama hicho alikuwa katika gari lake aina na Toyota Hiace aliteremka na kuwataka wanachama wake kuwa watulivu lakini hwakukubali ndipo polisi waliamaua kutumia nguvu kuwatanya. [3]
ama
Sidhani kama endapo ripoti ikitolewa na UN na nchi ikijiona ipo katika nafasi mbaya ama imeshika mkia itajisikia vizuri. [4]
ameanza
Pia Diwani mmoja wa CCM katika Manispaa ya Mwanza naye ameanza kujipitisha kwa wapiga kura kuwania jimbo hilo. [5]
ana
Kwa upande wa Jimbo la Mwanga linaloshikiliwa na Profesa Jumanne Maghembe nako kumekuwa na maneno ya chinichini ya kuwepo kwa msomi mmoja wa Chuo Kikuu cha Ardhi kuwa ana mpango wa kujitosa katika kinyang’anyiro hicho. [6]
au
Mbunge wa Ulanga Magharibi, Juma Ngasongwa anasema kuwa ni mapema kuzunguza iwapo atawania tena kiti hicho au la huku kukiwa na taarifa za baadhi watu wakiwamo watendaji wa juu serikali wanalinyemelea jimbo hilo. [7]
bila
Juhudi za kumtafuta waziri magufuli zilishindikana baada ya simu yake kuita muda mrefu bila majibu. [8]
bin
Wababe wa kivita walifanikiwa kuuondoa utawala wa kijeshi wa Kirusi hadi pale kundi la Watalebani lilipoitwaa nchi hiyo mwaka 1996. Utawala huo wa Watalebani ulifikia tamati mwaka 2001 kutokana na nguvu kubwa za kijeshi za Marekani, iliyokuwa ikimuunga mkono Osama bin Laden wakati huo. [9]
binamu
Mdogo wake, Amanullah alitwaa madaraka hadi mwaka 1929 madaraka yake yalipochukuliwa na binamu yake Nadir Khan aliyeongoza kwa miaka minne kabla ya kuuawa. [10]
bomu
Ili aamini kwamba kweli kuna mpango wa kulipua bomu ndani ya Nchi Tawala itabidi amwone huyu gaidi akiingia bungeni huko akiwa amebeba bomu mkononi. [11]
bwana
Shamba la Prince Benard ambalo aliuziwa bwana Ghandi miaka ya 1990, serikali imeanza mazungumzo ya kulinunua na mtapewa kuwa sehemu ya kijiji, " alisema Ndugai. [12]
chake
Tayari Sitta amenukaliwa hivi karibuni akilalamika kwamba mtu huyo amepandikizwa na mafisadi kwa ajili ya kumng'oa ubunge katika jimbo hilo ili kumkomoa kutokana na kitendo chake cha kuwabana mafisadi bungeni. [13]
chao
Alisema wamejitoa miongoni mwa watumiaji wa kanisa hilo kwa sababu wana kigango chao katika eneo jirani na lilipojengwa kanisa hilo. [14]
chongo
Kweli ushabiki ni chongo. [15]
dhana
Epuka dhana na kusikiliza maneno ya watu. [16]
doa
Wakati huo huo, kampeni CCM katika kusaka kiti cha udiwani nwa kata ya Kati jijini Arusha juzi ziliingia doa, baada ya baadhi ya wananchi kususia mkutano huo. [17]
dogo
Yanga iliwasajili wachezaji hao kutoka Tusker wakati dirisha dogo la usajili likiwa tayari limefungwa hivyo Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kuiwekea ngumu kutowatumia wachezaji hao kwenye michuano yoyote. [18]
dumu
Anasema kwa kawaida bei ya dumu moja huuzwa kwa sh. [19]
duni
Mama huyo ambaye ni mbunifu wa mitindo aliyedumu katika fani hiyo kwa muda mrefu zaidi, anasema elimu duni na kutoelewa umuhimu wa mitindo nchini ndiyo tatizo kubwa, kwani jamii ya kitanzania haina uelewa kabisa. [20]
es
Katika Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha anakabiliwa na upinzani mkubwa ndani ya CCM kutoka kwa mfanyabishara mkubwa kutoka Dar es Salaam ambaye ameonyesha nia ya kuwania jimbo hilo. [21]
eti
Tunaona ushabiki mtupu tunapoona hawa wanaojidai waumini wakitetea yasiyoteteka eti kwa sababu aliyetenda ni ‘mwenzetu’ wa dini yetu. [22]
faida
Tunampongeza Rais Kikwete kwa ufafanuzi huo alioutoa kwa mwekezi huyo, ambao pia ni kauli ya mwenye mali na karipio la kuwataka wasitumie vibaya madaraka yao kwa kufanya maamuzi ambayo hayana faida kwa taifa. [23]
familia
Siku hizo tatu zilimalizika Alhamisi iliyopita na watu mbalimbali wametoa ushahidi wakiwamo wanaume ambao walisema walibakwa mbele ya familia zao. [24]
fani
Wakizungumza na Mwananchi Jumapili kwenye kambi ya washiriki hao, walisema tangu mwanzo wamechukulia shaindano hili kama changamoto kwa mabinti walio katika fani ya muziki. [25]
gani
Kuna watu wananiuliza hivi nimeyajuaje haya mambo, wengine wauliza kama nimeolewa kwa muda gani kuweza kuyajua haya na wapo pia wanaotaka kujua kama naweza kuanzisha darasa kabisa. [26]
giza
Walisema watu hao maarufu kama Gamboshi nguvu zao za giza zilikuwepo kwenye eneo hilo katika kipindi cha miaka ya 1950, 1960 na 1980 lakini baadaye zilianza kupungua nguvu kwa kadri wamiliki wake walivyokuwa wakipungua kwa kufariki dunia. [27]
hadi
Moto huo wa uchaguzi unazidi kusambaa hadi mkoani Tabora ambapo Spika wa Bunge, Samuel Sitta naye ameshaanza kulialia kutokana na upinzani wa mganga wa kienyeji ambaye ameonyesha nia ya kugombea katika jimbo la Urambo Mashariki. [28]
haina
Pia Rais Kikwete aliinya TRL kwamba, reli ni mali ya serikali hivyo kampuni hiyo haina uwezo wa kuhamisha au kuirekebisha bila idhini yake na kwamba, hakuna sababu ya kuacha kutoa huduma katika baadhi ya njia za kwa vile hakuna abiria au mizigo ya kusafirisha. [29]
haja
Anaongeza kwamba, ipo haja ya kutoa elimu kwa walengwa wabunifu ili waweze kufanya kazi zao vizuri na kwa tija zaidi na hatimaye kuwasaidia kujikwamua kiuchumi kama wanavyofanya jirani zetu wa Kenya na Uganda. [30]
hapo
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), kimeongeza muda wa wanafunzi kutuma upya maombi ya udahili chuoni hapo, hadi Januari 29 mwaka huu. [31]
hasa
Jimbo la Muleba Kusini linaloshikiliwa na Wilson Masilingi anakabiliwa na upinzani wa dhahiri kutoka kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es Salaam, Alfred Tibaigana, huku mbunge huyo akigeukwa na baadhi ya wanaCCM na hasa madiwani wa wilaya hiyo. [32]
hatua
Kashfa hizo zilisababisha wananchi kupunguza imani kwa serikali na viongozi wao, huku wakidai kufanyika kwa uchunguzi zaidi na wahusika wa mikataba hiyo mibovu na wizi wa fedha za EPA wachukuliwe hatua za kisheria. [33]
hauna
Wakati Mukandala akisisitiza hivyo aliyekuwa Rais wa Daruso, Anthony Machibya amepingana na kauli hiyo na kusema, wao bado ni viongozi halali na wenye mamlaka hivyo uongozi wa chuo hauwezi kuwafuta kwa kuwa hauna mamlaka hayo. [34]
hayana
Kwa upande mwingine majimbo yanayoelezwa kuwa hayana upinzani mkali ni Kilosa linalishikiliwa na Mustafa Mullo ambaye pia ni Waziri wa Fedha, na Ulanga Mashariki lililo chini ya Celina Kombani ambaye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. [35]
hayo
Wakati Mvomero yanaripotiwa hayo, katika Jimbo la Morogoro Mjini linaloshikiliwa na Dk Omary Mzeru inaelezwa kuwa Meya wa Manispaa hiyo, Romanus Ishengoma anatajwa kulinyemelea jimbo hilo. [36]
hewa
Alieleza kuwa upandaji miti ni muhimu kwa vile inaweza kutumika kama njia nzuri ya kudhibiti mabadiliko ya tabianchi na hewa chafu ambavyo kwa pamoja huchangia uchafuzi wa mazingira hasa upande wa ongezeko la joto duniani na uharibifu wa tabaka la Ozoni. [37]
hii
Unajua ibada zetu zinakuwa na utaratibu wake na wala dini siyo kitu cha kutengeneza bali ni kitu cha kiroho zaidi, ukiwa katika kanisa hilo huwezi kupanga maendeleo yako na kanisa lako, maana hilo ni la watu wengi, lakini pia kunaweza kuzuka ugomvi wa nani amlipe mlinzi au nani afanye usafi, hii siyo hoja isipokuwa kunaweza kuibuka malumbano ya kiimani, kwamba hawa wanatumia msalaba au mambo mengine," alieleza Paroko. [38]
hiki
Hili tukio limetushtua sana na kwa kweli hakuna ajuaye limesababishwa na nani lakini kama wazee wa kijiji hiki wanavyodai, eneo hili limebaki kama historia kwa sababu inasemekana ilikuwa ngome kuu ya watu wanaojihusisha na vitendo vya kishirikina," alisema. [39]
hilo
Hali hiyo imetafsiriwa na viongozi wa CCM na wananchi wa Jimbo hilo kuwa ni dalili za kujipitisha mapema kwa wapiga kura na kumshangaa kwa kauli yake kwa hiyo hakuwahi kusimama majukwaani kama mgombea na kutoa ahadi. [40]
hisa
Kwa mujibu wa Kikwete, serikali ambayo inamiliki hisa 49 na kampuni ya Rites ya India yenye hisa 51, ndiyo wamiliki wa TRL, hivyo menejimenti yake haitakiwi kufanya maamuzi yoyote makubwa bila kuwashikirisha ili wajue kinachoendelea na kutoa maoni yao, badala ya kupewa taarifa za utekelezaji tu. [41]
hizi
Mchuuzi mmoja wa maji Ludovick Temu, aliyezungumza na mwandishi wa habari hizi alisema kwa kipindi cha wiki ameweza kujiongezea kipato kwa siku kwa kupata zaidi ya sh. [42]
hizo
Majimbo mengine yanayoonyesha wabunge wa sasa kupata upinzani ndani ya CCM mkoani humo ni pamoja na Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Morogoro Kaskazini Mashariki huku mbunge wa zamani Semindu Pawa na Azizi Abood wakitajwa kutaka kutaka kuwania nafasi hizo. [43]
hofu
Akizungumza na Mwananchi Jumapili jijini Dar es Salaam jana Ngasongwa alisema "Wanaotaka kuwania jimbo langu wapo huru, hawanitii hofu. [44]
huamua
Watu wengi wanaona kwamba, kuzingatia mitindo ya mavazi katika uvaaji hakuna maana na hatimaye huamua kuvaa wanavyotaka na matokeo yake watu wanavaa nguo zisizoendana na matukio au mahali husika. [45]
hujui
Kwa kuwa hujui aliyekuletea ana nia gani na mumeo. [46]
hujuma
Kwa kutumia mwanya huo huo wa serikali kulala kusimamia mambo mengi muhimu, watumishi wengi wa umma wamejipata madaraka ya kufanya mambo ambayo kwa uhakika ni hujuma dhidi ya serikali yao. [47]
huo
Hata hivyo, Owenya mwenyewe akizungumza kwa simu na Mwananchi Jumapili kutoka Uholanzi, aliukana waraka huo akisema ni wa kugushi na kwamba hajafikiria wala kujipanga kuwania ubunge wa jimbo hilo kama waraka huo unavyodai. [48]
huu
Ni wazi kuwa historia ya matukio hayo, CCM inaweza kupata hukumu mbaya kutoka kwa wapiga kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwaka huu na hata uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ya kukataliwa na wananchi,"alisema. [49]
huwa
Tunalazimika kutumia maji ya visima na ya mto ambayo sio safi wala salama, hali hii ni hatari kwani licha ya wauzaji wa maji kuyauza maji kwa bei mbaya lakini hata upatikanaji wake huwa mgumu licha ya kuyanunua kwa kati ya sh. [50]
huyu
Hivi sasa mama huyu ameolewa na ana watoto wanne, watatu wakike na wa kiume mmoja. [51]
ibada
Paroko wa Parokia ya Chato, Padri Ladislaus Mwilinde amekiri kanisa lake kukataa kutumia kanisa hilo kwa ibada zake za kawaida. [52]
idadi
Machibya pia alishangaa waziri huyo pamoja na Profesa Mukandala kueleza kuwa wanafunzi wengi wametimiza masharti bila kutoa idadi yao kitu ambacho kinaonyesha kutokufanyika vitu kwa umakini. [53]
ijayo
SHINDANO la Malikia wa Sebene 'Ngwasuma' inafanyika Ijumaa wiki ijayo, kwenye Ukumbi wa New Msasani Club. [54]
ikawa
Na inawezekana ikawa hujui nini kamwambia mumeo kuhusu wewe. [55]
ikiwa
Asia Idarous ambaye ni mkongwe katika fani ya ubunifu wa mitindo hapa nchini, anasema hiyo fani inayoweza kutumika kama shughuli ya kujikwamua kiuchumi, ikiwa muhusika atakuwa makini katika kufanya kazi zake. [56]
ila
Anselim ambaye ni mwenyekiti wa kwanza wa kijiji hicho, kilichoanzishwa mwaka 1972, alisema wananchi hawapingani na serikali, ila wanalalamika kutokana na maamuzi kutolewa bila wao kushirikishwa. [57]
ili
Kumekuwepo na propaganda zinazoenezwa na hata baadhi ya viongozi wa CCM kuwa Profesa Maghembe amuamua kutogombea tena 2010 ili kumuachia msomi huyo, kauli ambazo zimekanushwa vikali na waziri huyo na kuwataka wapiga kura wake kuzipuuza. [58]
imara
Kipa wa JKT, Abdallah Ngachimwa alisimama imara na kuokoa shuti la Ambani katika dakika ya 22 kabla ya Kessy Muhsin kupiga shuti la umbali wa mita 30 lililodakwa kifundi na Juma Kaseja. [59]
in
Nilianzisha rasmi utaratibu wa kuonyesha mitindo ya mavazi mwaka 1986. Mara ya kwanza zaidi ya wanamitindo kumi walipanda jukwaani kunadi mavazi yangu,” anafahamisha na kuongeza kuwa hadi kufikia wakati huu, ameishafanya maonyesho 71 na kwamba, February 6,2009 anatarajia kufanya onyesho la 72 litakalofahamika kama Lady in red, likiwa maalum kwa sikukuu ya wapendanao (Valentines day). [60]
internet
Kuna baadhi ya wasomaji wataanza kujiuliza e-government ni nini? Hizi ni huduma ambazo zinatolewa na serikali kwa wananchi wake kwa njia ya kompyuta ambayo imeunganishwa katika mtandao wa internet. [61]
ipo
Hii ramani ilikuwa ni mapendekezo ya zamani ya Tanapa, lakini suala hili halipo msiwe na hofu, mimi ndiye Naibu Waziri na mamlaka hiyo ipo chini yangu," alisema Maige. [62]
je
Haya, na hapa je? Mimi sikatai ni dhahiri kwamba wanene wa mafuta walitaka kutunyonya mwisho. [63]
joto
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira naye anakabiliwa na upinzani mkubwa ndani ya chama hicho lakini joto kali la upinzani linatoka kwa Chadema. [64]
jumla
Akitoa taarifa hizo, Ibrahimu alisema kuwa katika kipindi hicho jumla ya vikongwe 179, waliuawa. [65]
juzi
Kamati hiyo ambayo juzi imepokelewa kwa mabango na wananchi wa Kijiji cha Mayo Mayoka ambao walikuwa wanapinga azimio la bunge la kupanua hifadhi hiyo wakihofia kuhamishwa, ilitumia muda mrefu kufafanua maamuzi hayo ya bunge. [66]
kamati
Mamia ya wananchi wa kijiji hicho, walijitokeza katika mkutano wa kamati hiyo uliofanyika katika Kijiji cha Mayo Mayoka. [67]
kambi
Siku chache kabla ya kushinda kesi, Zuma alifanya ziara hapa nchini kwa kufanya vikao na viongozi kadhaa ndani ya CCM pamoja na kutembelea kambi mkoani Morogoro, zilizokuwa zikitumiwa na ANC katika harakati za ukombozi wa nchi hiyo. [68]
karne
Ukiachilia mbali himaya mbalimbali zilizokuwa zikipigana kikumbo kuitwaa Afghanistan, karne ya 19 ilishuhudiwa mapambano mengi zaidi kutokana na mataifa yenye nguvu kujikita zaidi katika kujipanua na kulinda maslahi yao katika Asia ya Kati. [69]
kasi
Kipindi cha pili, Yanga waliongeza kasi ya mashambulizi na katika dakika ya 67, Shamte Ally aliipatia bao kwa kichwa baada ya kuunganisha krosi ya Mrisho Ngassa. [70]
kiasi
Alisema taarifa za kuwepo kwa mafuvu hayo ziliwashutua wakazi wa kijiji hiocho pamoja na vile vinavyokizunguka kiasi cha kuwafanya Wengi kumiminika kwenda kushuhudia. [71]
kidedea
KOCHA Mkuu wa timu ya Polisi Morogoro John Simkoko ametamba kuibuka kidedea katika mchezo wao dhidi ya Simba ya jijini Dar es Salaam timu hizo ambazo zitakutana leo katika Uwanja wa Taifa jijini. [72]
kidogo
Hadi awamu ya kwanza ya programu hiyo ilipomalizika mwaka jana, mafanikio yaliyopatikana na kidogo. [73]
kigaidi
Kwa sasa, Majeshi ya Umoja wa Kujihami wa nchi za Magharibi (Nato) yanakalia sehemu kubwa ya nchi hii kwa madai ya kutaka kuyaondoa makundi ya kigaidi ya Al – Qaeda. [74]
kila
Alisema baada ya kukabidhiwa jengo hilo na Waziri Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato, walipangiana utaratibu wa kulitumia kwa kufuata muda maalum ili kila kanisa liweze kunufaika, lakini makanisa mengine walijitoa. [75]
kile
Mbunge wa Kahama, James Lembeli naye anavutana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja kwa kile ambacho kinadaiwa kuwa ni ugomvi unaotokana na kugombea uvunge. [76]
kipindi
Aidha katika kipindi hicho cha mwaka 2008 taifa lilishuhudia kuingia kwa mustakabali uliozusha mjadala wa Zanzibar ni nchi au la ulioliopandisha joto katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuzua hofu ya mpasuko katika muungano huo. [77]
kitakuwa
Naye mkurugenzi wa msanii huyo, Hartmann Mbilinyi anasema Steve anatarajia kutengenezewa kipindi ambacho kitakuwa ni fungakazi kwa sanaa ya vichekesho ambayo inaonekana kupata umaarufu mkubwa hapa nchini. [78]
kocha
Akizungumzia mchezo huo, kocha wa JKT Ruvu, Charles Kilinda alisema ngome kukosa umakini ndiyo chanzo cha wao kufungwa. [79]
kona
Mabao ya Mtibwa yaliwekwa kimiani na Rashid Gumbo katika dakika 20 na Abdallah Juma katika dakika 89 baada ya kuunganisha mpira wa kona wa Yahaya Akilimali. [80]
kote
Mimi sikisemi chama chochote kile maana ushabiki huo uko kote kote, kwa chama cha zama zile hadi chama cha zama hizi. [81]
kuacha
JUZI Rais Jakaya Kikwete aliutaka uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kuacha kuchukua maamuzi makubwa katika uendeshaji wa kampuni hiyo bila kuishirikisha serikali ambayo ni mwanahisa muhimu. [82]
kuamini
Fyatu mwenzio wa Marekani, Michael Moore, alisema kwamba baada ya kuambiwa uongo mwingi kuhusu silaha za maangamizi na kadhalika, hawezi kuamini neno lolote linalotolewa na serikali yake. [83]
kuchokwa
Afadhali hata mpira maana hatimaye mashabiki wataanza kudai mabadiliko lakini katika siasa, watu watashabikia weeeeeeeeeeeee huku chama fulani kimeshapondwa badala ya kupendwa, kimechekwa na kuchokwa na hata kuchukiwa kutokana na kuchakaa kwake. [84]
kuingia
Mmoja wa waumini hao, Zacharia Gabriel alisema kutokana na kuwepo kwa msalaba ndani ya kanisa hilo baadhi ya waumini wa Kipentecoste nao waligoma kuingia katika kanisa hilo hali ambayo imepunguza waumini wanaosalia humo hadi 20 kila Jumapili. [85]
kuinua
Mashindano hayo ambayo yanalengo la kutafuta vipaji kwa vijana kwa ajili ya kushiriki mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ikiwemo ya Jumuiya ya Madola pia yamelenga kuinua mchezo huo hapa nchini. [86]
kuitwaa
Historia ya taifa hilo kuendelea kuvamiwa kwa sababu za kujiimarisha kivita kwa mataifa yenye nguvu, inaonyesha kuwa mataifa mengine mengi yalijitokeza kutaka kuitwaa nchi hiyo. [87]
kujaribu
Kujua na kujaribu kutumia njia sahihi ya kugombana kutasaidia kutatua migogoro yenu. [88]
kujua
Hivyo UN ikaona kuna haja ya kufanya utafiti ili kujua nchi zilizopiga hatua katika matumizi ya kompyuta na internet katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi wake na zenye ubora. [89]
kulia
Shadrack Nsajigwa anacheza kulia huku kushoto kocha akitarajia kumchezesha yoyote kati ya Nurdin Bakari, Abuu Mtiro kutokana na Amir Maftah kuumia katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Zesco ya Zambia juzi. [90]
kumsikiliza
Ongeza umakini katika kumsikiliza. [91]
kundi
Pamoja na hayo kundi la wana mtandao linalodaiwa kuwa ndilo lililomwingiza madarakani Rais Kikwete lilidaiwa kugawanyika katika makundi mawili, yaani wanamtandao wasafi na wanamtado wanaodaiwa kujihusisha na ufisadi. [92]
kutuma
Naye Mchungaji, Kivuyo alisema kabla ya bunge kufikia maamuzi lilipaswa kutuma wajumbe katika maeneo hayo kuzungumza na wananchi. [93]
kuu
WAZEE wa Kijiji cha Manyaji wilayani Kishapu mkoani hapa wamedai kuwa eneo ambalo yamegundulika mafuvu 40 ya binadamu ni ngome kuu ya wachawi ambayo walikuwa wakiitumia kuwahifadhi watu wanaowachukua kimazingira wakiwa hai, maarufu kama misukule. [94]
kuvamiwa
Taifa hili la Kiislamu linaloongozwa na Rais Hamid Karzai, linalokadiriwa kuwa na jumla ya watu milioni 32.7, ikiwemo wengine milioni 3.5 wanaoishi kama wakimbizi huko ughaibuni, lilianza kuvamiwa na Himaya ya Median (Iran) iliyojipanua na kuingia katika eneo la nchi hiyo miaka 700 kabla ya kuzaliwa Kristo. [95]
kuwapo
Alisema kutokana na kuwa na kigango chao jirani na eneo hilo na kuwapo mipango ya kujenga jingine wameamua kutolitumia kanisa hilo kwa utaratibu wa ibada zao. [96]
kuzidi
Lakini mara nyingi kunyamaza ni kuzidi kuzidisha matatizo. [97]
kwake
Kuwepo kwa upinzani mkali katika jimbo hilo ndiko kulikosababisha hivi karibuni baadhi ya wananchi wa jimbo hilo kupiga mawe msafara wake uliohusisha magari ya halmashauri na baadhi ya watuhumiwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani, ingawa yeye amekanusha vikali kuwa na msafara wa magari ya serikali usiku na kupigwa kwake mawe. [98]
kwao
Kaimu Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Mayanji, Peter Makaranga, alikiri kuwepo kwa matukio ya watoto wadogo kufariki dunia katika mazingira ya kutatanisha na baadaye kuwepo kwa taarifa za kuonekana kwao wakiwa hai. [99]
la
Ugomvi wa hivi karibuni kabisa wa kati ya Mbunge wa Jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, James Ole Millya ambao umesababisha mbunge huyo kutinga mahakamani ni mfano tu wa moto unaowaka katika majimbo mengi nchini. [100]
leo
Hapa unaniona naendesha mafundisho ya biblia, haya ni moja ya matunda ya kanisa hili, awali hatukuwa tukifika huku, lakini leo ibada imefika tunasali," alieleza Mwinjilisti huyo. [101]
licha
Utata wa kanisa hilo umekuja kutokana na waumini wa Kanisa Katoliki na wenzao wa AICT kukataa kulitumia kwa sababu mbalimbali ikiwamo ya tofuati za taratibu za kusali licha ya kwamba walikabidhiwa kanisa hilo walitumie kwa pamoja. [102]
ligi
Naye Dorice Malyaga anaripoti kuwa Mtibwa Sugar imeichapa Kagera Sugar mabao 2-1 katika mchezo wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani. [103]
lile
Alisema ingawa kanisa hilo limejengwa kwa ajili ya matumizi ya wote, madhehebu mengine yamejitoa kutokana na sababu za kiimani na lile la kutumia na watu wa madhehebu tofauti. [104]
lolote
MALIPO ni ya jambo lolote hapa hapa duniani. [105]
lukuki
Tuchukue mfano wa wale ambao wamenyang'anywa nchi yao miaka 60 iliyopita na kunyanyaswa ndani ya nchi hiyohiyo miaka yote hii, hadi sasa wanapodondoshewa mabomu yanayoua watoto lukuki kila siku. [106]
maadui
Pamoja na Hamid Karzai kuelezwa kwamba amewekwa madarakani na Wamarekani, bado utawala katika baadhi ya maeneo ni mgumu kutokana na Watalibani hao kujikikita sawa sawa wakionyesha kuwa tayari kupambana na maadui zao wanaotaka kulifuta kundi hilo linalolaumiwa kwa biashara ya mihadarati. [107]
mafuta
Kivipi? Kama unavyojua kusema maneno yanayoudhi ni kama kumtupia kijinga cha moto mtu ambaye tayari ameshaoga mafuta ya taa. [108]
mantiki
Kwa mantiki hiyo, itakuwa kinyume cha sheria kwa mwanafunzi yeyote kufanya chochote kile kwa kisingizio cha kuwa kiongozi wa wanafunzi aliyechaguliwa," alisema Mukandala. [109]
mara
Ikiwa Kikwete atawania urais kwa mara ya pili uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 atalazimika kuzingatia hali halisi na historia iliyoukumba utawala wake katika miaka mitatu ya mwanzo na kuhitaji kujipanga upya," alionya mwanasiasa huyo. [110]
masomo
Kwa mujibu wa uongozi wa chuo hicho uamuzi huo unalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi kukamilisha uwasilishaji wa kiwango cha ada wanachostahili, kutoa kwa mwaka wa masomo 2008/09 kabla ya kuruhusiwa kujiunga na masomo katika muhula huu. [111]
matukio
Kulazimika kwa Kikwete kufanya mabadiliko hayo kunatokana na matukio ya ufisadi yaliyoikumba mwaka jana na kuwahusisha baadhi ya watendaji wake wakiwamo mawaziri. [112]
mazuri
Kocha huyo alisema timu yake ilikuwa katika maandalizi mazuri ya ligi na wachezaji waliingia kambini muda wa mwezi mmoja kabla ya mzunguko kuanza huku wakicheza michezo mbali mbali ya kujipima nguvu na wanaamini kwa mazoezi hayo yatawafanya wao kuwa timu ya kutisha katika mzunguko huu. [113]
mbali
Kesi hiyo ambayo ilitupiliwa mbali na Mahakama Kuu ya nchi hiyo, ilikuwa inatishia uwezekano wa Zuma kuwa rais kwenye uchaguzi utakaofanyika mwaka huu. [114]
mbele
Maafande hao wa JKT watakuwa wakiwatumaini Bakari Kondo, Sostenes Manyasi, Haruna Adolph,Rashid Matambo, George Minja na Kessy Mapande kuhakikisha Yanga haifurukuti mbele yao na wanatoka na pointi tatu muhimu. [115]
mbio
MASHINDANO ya mbio za baiskeli mkoa wa Pwani yanatarajia kufanyika leo wilayani Kibaha na yatashirikisha wakimbia kwa baiskeli kutoka Jijini Dar es salaam na Mlandizi. [116]
mdogo
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa kutokana na umuhimu wa jambo hilo, Kikwete anaweza kufanya mabadiliko katika baraza lake la mawazri wakati wowote kuanzia sasa ili kuondoa makapi na kupata timu bora na safi ya watendaji itakayombeba yeye na CCM katika uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu. [117]
mgeni
ALIYEKUWA Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki, jana alikuwa ni mgeni rasmi katika kongamano la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CCM) lililofanyika Zanzibar. [118]
miche
Kwa mujibu wa Mwangunga, tatizo kubwa linalozitia doa kampeni za upandaji miti na hata mwamko wa wananchi kupenda kupanda miti ni upatikanaji mdogo wa miche ya kutosha. [119]
minne
Ripoti hiyo ya miaka minne iliyopita inaonyesha kuwa Tanzania imeshuka kutoka nafasi ya 127 mwaka 2005 hadi 147 mwaka jana. [120]
mipya
Anasema awali alikuwa anabuni mitindo ya mavazi kwa ajili ya watu binafsi na baadaye alianzisha maonyesho ya mavazi kwa lengo la kuonyesha mitindo mipya aliyobuni. [121]
miti
JANUARI Mosi mwaka huu ilikuwa ni siku ya taifa ya kupanda miti. [122]
mitindo
FANI ya mitindo imekuwa ikichukuliwa kama burudani, hasa pale wabunifu wanaponadi kazi zao, kitendo ambacho kimekuwa kikichangia kupotosha maana yake halisi. [123]
mkazi
Mama Fita mkazi wa Kimara mwisho. [124]
mkopo
MABINGWA wa Soka Tanzania Yanga, tayari wameanza mazungumzo na timu ya Tusker ya Kenya kwa ajili ya kuwapeleka kwa mkopo wachezaji wa zamani wa timu hiyo Joseph Shikokoti na John Njoroge. [125]
mto
Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya wakazi wa maeneo hayo wamesema wapo katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na kulazimika kutumia maji ya visima na ya mto ambayo sio salama kwa afya za watumiaji. [126]
muda
Akijitokeza mtu na kumwona anafaa kuwania kiti hicho nipo tayari kumuachia, lakini muda wa kuzungumza iwapo nitagombea au la bado. [127]
mumeo
Kubeba ulichoambiwa ukakitumia kama fimbo ya kumhukumu mumeo ni makosa makubwa. [128]
mwa
Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili katika mikoa mbalimbali nchini, umebaini kuwa yameshaanza kujitokeza mambo mbalimbali ya chinichini na ya wazi, yakaiwamo malumbano na ugomvi usiokoma miongoni mwa wanasiasa yanayosababishwa na kinyang’anyiro hicho. [129]
mwezi
Alisema katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka huu, wilaya ya Bukombe imekuwa na mauaji ya vikongwe 15, Bariadi 13, kahama 12, Meatu 3, Kishapu 2, shinyanga 1 na Maswa kulikuwa shwari. [130]
mwingi
Ugomvi mwingi wa wanawake wengi unatokana na maneno ya kuambiwa ama kudhania. [131]
na
IKIWA imebakia takribani miezi 22 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2010, vita vya chinichini vya kuwania majibo vimeanza huku baadhi ya wabunge wa sasa wakiwamo mawaziri wakikabiliwa na upinzani mkali katika kutetea viti vyao. [132]
nao
Kanisa Katoliki walijitoa kutokana na utaratibu wao wa ibada kutofautiana na makanisa mengine, AICT wao walidai hawana maono ya kuhusiana na matumizi ya kanisa hili, hivyo nao kuamua kukaa pembeni," alieleza Mahugi. [133]
naye
Mbali na Mmasi lakini Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Owenya wa Chadema naye anatajwa kuwania Jimbo hilo na kumekuwepo na waraka wa siri unaodaiwa ni wake (nakala tunayo), unaosambazwa kwenye mtandao wa kompyuta ukielezea mkakati madhubuti wa kulitwaa jimbo hilo. [134]
nayo
Akiwazunguzia Simba alisema ni timu nzuri kwani wanawaelewa kwa kupitia michezo yao mbalimbali waliyoiona lakini kwa staili yao mpya waliyoanza nayo wanaamini watafanikiwa kutika na ushindi kupitia kwa wekundu hao wa msimbazi. [135]
ndipo
Alisema awali walimpeleka Pius Msekwa kwa kazi hiyo, lakini wakaona hawezi kuwashawishi wananchi ndipo wakamgeukia Malecela ambaye pia hana uwezo huo. [136]
ndiyo
Serikali ya Mkapa ndiyo iliyoidhinisha fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uwanja wa ndege wa Songwe, lakini serikali hii imeutelekeza kwa nia ya kumkomoa Prof Mwandosya, hawajui kama kufanya hivyo ni kuwakomoa wananchi wa Mbeya Vijijini na mikoa jirani ambao ndiyo wangenufaika na uwanja huu,"alisema. [137]
ngazi
Viongozi hao wa ngazi ya kitaifa waliowasili jana pamoja na Mweyekiti wa CUF Taifa, Prof Ibrahimu Lipumba ni Augustino Mrema wa TLP na Peter Mzirai PPT Maendeleo. [138]
ngumu
Aidha Mbogoro alisema kuwa endapo watashinda kwenye kesi hiyo ana imani CCM itakuwa kwenye hali ngumu kwani viwanja vyote nchini ambavyo vinamilikiwa na chama hicho kama CCM Kirumba Mwanza, Sokoine Mbeya , Jamuhuri Dodoma na Morogoro, Mkwakwani Tanga , Ally Hassani Mwinyi Tabora, Amri Abeid Arusha na Samora Iringa vyote vitakuwa mali ya wanachi hivyo watakosa vyanzo vya mapato. [139]
ni
Wengi wa wabunge hao ambao ni wa Chama cha Mapinduzi(CCM), wanakabiliwa na upinzani wa aina mbili wa kwanza ukiwa ni wa kutoka ndani ya CCM yenyewe na mwingine kutoka kwa wagombea wa upinzani unaotokana na kuimarika kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). [140]
nini
Kama unavyojua vigezo vya kushiriki shindano hili siyo urembo bali ni kipaji alichonacho mtu katika kucheza kwa ufasaha na kwa bahati nzuri sote tunafundishwa sawa na mwalimu kutoka katika bendi hivyo, sioni ni nini kitatushinda kuonyeshana kazi" alisema mmoja wa washiriki hao. [141]
of
Akizungumza jana na Mwananchi Jumapili, Mchungaji Reuben Mahugi wa Kanisa la Free Pentecost Church of Tanzania (FPCT) ambaye ndiye msimmizi mkuu wa matumizi yake kwa sasa, alisema kanisa hilo limekuwa likitumiwa na makanisa mawili, la kwake na Anglikana baada ya makanisa mengine kujitoa. [142]
ofisi
Akizungumza baada ya kuwasil katika ofisi za CUF, Wilaya ya Mbeya Wijijini, Prof Lipumba alisema wameenda kuongeza nguvu na kuhakikisha kuwa anapatikana mbunge anayeweza kuwatetea wananachi na wakulima wa jimbo la Mbeya vijijini maendeleo kwa kuwa wamechoka na ahadi za uongo za Chama Cha Mapinduzi (CCM). [143]
pale
Mchezo wa jana ulikuwa wa mashambulizi ya hapa na pale, na Yanga walilifikia lango la wapinzani wao katika dakika za 15 na 30 lakini Jerry Tegete na Boniface Ambani mashuti yao hayakulenga lango. [144]
pekee
Hili si katika serikali pekee bali hata katika makampuni binafsi, mashirika na taasisi mbalimbali. [145]
pia
Mbali ya kukabiliwa na upinzani kutoka ndani ya CCM, pia mfanyabiashara mmoja jijini Mwanza anadaiwa kuanza kujindaa kwa ajili ya kugombea kupitia Chadema. [146]
poa
Na kwa kuwa Makengeza Enterprises haitaki watu wapekue baadaye na kupata funza badala ya mafunzo, viatu maalum vitauzwa kwa bei poa hapohapo kwenye tamasha. [147]
polisi
Mara baada ya msafara huo kufika katika Barabara ya Sokoine, magari mawili ya polisi aina ya Land Rover yalifika yakiwa yamesheheni askari, wakausimamisha bila mafanikio kisha vurugu hizo zikaanza. [148]
rafiki
Bemba ni mmoja kati ya wafanyabiashara maarufu nchini Kongo, baba yake Jeannot Bemba ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa Dikteta Mobutu Sese Seko naye alikuwa tajiri mkubwa wa wakati huo. [149]
rais
Mbeki ambaye alikuwa rais aliyepokea madaraka hayo kutoka kwa shujaa kwa kumaliza ubaguzi wa rangi nchini humo, Mzee Nelson Mandela, alilazimika kujiuzulu mwaka jana kutokana na shinikizo la chama chake cha African National Congress (ANC). [150]
ramani
Naye Maige alisema yeye kama kiongozi wa wizara hatambuwi jambo la kuhamishwa wananchi kutokana na upanuzi wa hifadhi hiyo huku akiikana ramani ya Mamlaka ya Mbuga za Wanayama za Taifa (Tanapa). [151]
ripoti
UTAFITI uliofanywa hivi karibuni na Umoja wa Mataifa (UN) kuhusiana na masuala ya e-government na ripoti yake kutolewa mwaka jana, Tanzania imeshuka kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na mwaka 2005, ripoti hiyo ilipotolewa mara ya mwisho. [152]
saa
Ratiba iliyowekwa awali ilikuwa ni kuanza kutumiwa na wakatoliki kuanzia saa 2:30 hadi 4:00 asubuhi, FPCT kuanzia saa 4:00 hadi saa 7:00 mchana na kisha Anglikana kuanzia saa 9:00 alasiri hadi saa 11:00 jioni. [153]
safi
Kikwete sasa amechoka na kuchafuliwa na watendaji wake anataka kuwa na timu safi ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao," alidokeza mwanasiasa mmoja nchini aliyepo karibu na Kikwete. [154]
sanaa
Anasema yeye binafsi amepania kuboresha sanaa yake na kuipenyeza katika soko la kimataifa. [155]
sawa
Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Umma (Uvijuta), Silinde David, alisema wanafunzi waliofukuzwa vyuoni walikuwa ni 31,443 na hadi hivi sasa walioweza kulipa ni asilimia 13 ya wanafunzi hao huku asilimia 87 ambayo ni sawa na wanafunzi 27,289 hawajalipa. [156]
sekta
Maadhimisho ya siku hiyo yaliyoanza kuadhimishwa mwaka 2001 yamekuja huku kukiwa na taarifa kuwa sekta ya misitu imekuwa ikikabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo upoteaji wa miti. [157]
sera
Vile vile sababu nyingine ambayo inasababisha teknolojia hii muhimu kutotumika ipasavyo ni pamoja na kukosekana kwa sera na mipango madhubuti ya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama), katika taasisi za serikali. [158]
sh
Huku wakazi wa maeneo hayo wakitaabika, wachuzi wadogo wameonekana kujipatia kipato kwani hununua maji hayo kwa wauzaji wa magari na kisha kuyauza reja reja kwa ndoo moja kwa kati ya sh. [159]
shamba
Ndugai alisema serikali inatambua tatizo la ardhi katika kijiji hicho, hasa baada ya upanuzi wa hifadhi na kwamba, kijiji pia kitapewa eneo la shamba la Prince Benard kuwa sehemu yake. [160]
si
Hapana shaka Yanga leo ina kila sababu ya kuibuka na ushindi kutokana na silaha zake zote zilizokuwa timu ya Taifa kurejea tayari kwa mchezo huo licha ya kuwa JKT Ruvu nayo si timu ya kubeza. [161]
sifa
Kwa hiyo, kwa sifa ya Tanzania ilivyo, tangu eeeeenzi za mwalimu, tutasimama upande gani? Upande wa wanaonyanyaswa. [162]
sio
Hatukuvunja utaratibu kwani tulikuwa tumetoka katika mkutano wa hadhara kuelekea Kaloleni, lakini polisi walipigiwa simu na wafuasi wa CCM wakidai kuwa tunaleta fujo kitu ambacho sio cha kweli," alisema Simba. [163]
sisi
Nilifikiri sisi tulikuwa tunanyanyaswa lakini nilichoona huko ni zaidi. [164]
soko
Idarous anapendekeza kuwa vianzishwe vyuo vya ubunifu wa mitindo katika ngazi mbalimbali ili kupata watu wenye ujuzi kamaili ambao wataweza kutengeneza bidhaa zitakazoweza kushindana katika soko la kimataifa. [165]
tabia
Kwa upande wake mgeni rasmi Diwani wa kata ya Majengo Iddi Abdalah amelipongeza shirika hilo kwa kutoa mafunzo hayo yatasaidia kuleta mabadiliko ya mtazamo,tabia na mwenendo uliobora kwa vijana. [166]
tamko
Kwa upande wake Mwenyekiti chama cha PPT Maendeleo, Mziray alikitaka ChamaDemokrasia na cha Maendeleo (Chadema) kutoa tamko la kuinga mkono CUF katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya vijijini mapema kabla ya uchaguzi huo kufanyika ili baadaye kisije kujuta. [167]
tatu
Kutokana na matukio hayo, Rais Kikwete alilazimika kulivunja baraza lake la mawaziri na baada ya siku tatu aliunda baraza jipya la mawaziri pamoja na kubadilisha muundo wa baadhi ya wizara na nyingine kuziunganisha huku Mizengo Pinda akiteuliwa kuwa Waziri Mkuu. [168]
tuna
Ni kweli tuna mpango wa kuwarudisha Tusker kwa mkopo na mazungumzo tayari yameanza ila yapo katika hatua ya awali tutaendelea kuwafahamisha yakikamilika" alisema Madega. [169]
ubora
Kabla ya kutoa ripoti hiyo, UN huangalia idadi ya huduma zinazotolewa na serikali husika kwa wananchi wake kwa njia ya kompyuta ambayo imeunganishwa na mtandao wa internet ikipima kwa vigezo vya ubora wa huduma hizo. [170]
uhuru
Ninaye rafiki yangu ambaye alikuwa mpigania uhuru wa Afrika Kusini. [171]
ujao
Inaelezwa kwamba Operesheni Sangara ya Chadema imevunja mizizi mingi ya CCM katika jimbo hilo na hivyo mgombea wa chama hicho katika uchaguzi ujao atapata upinzani ambao hakutarajia. [172]
uko
Mkoani Kagera, upinzani wa Naibu Katibu Mkuu Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare dhidi ya Mbunge wa Bukoba Mjini Hamis Kagasheki ambaye pia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani bado uko moto na habari zinasema kuwa anajiandaa kichini chini kuchukua tena jimbo lake baadaya ya kumuonyesha makeke katika uchaguzi wa mwaka 2005, kutawaliwa na vurugu na madai ya wizi wa kura. [173]
unyama
Enzi zile, daima alinielezea unyama wa makaburu, unyama wa kutisha. [174]
upo
Stive Nyerere nimemuandalia mipango ya mwaka mpya ambayo itakuwa na mafaniko makubwa katika sanaa yake, kwani kutokana na uzoefu wangu katika nchi nyingi za Ulaya nilizotembelea, hivyo naamini kuwa uwezo wa kukamata soko la dunia upo," anasema Mbilinyi. [175]
viatu
Kutakuwepo na sanamu kubwa ya Kichaka na wote mtapewa nafasi ya kuitupia viatu kwa nguvu zote. [176]
vikosi
Inadaiwa kuwa kati ya mwaka 2002 na 2003 vikosi vya jeshi vya Kongo vilivyotumwa na Bemba nchini humo vilifanya ubakaji, unyanyasaji na mauaji. [177]
vile
Vile vile alisema kanisa lake limeamua kutolitumia kanisa hilo kutokana na kuwa na taratibu tofauti za ibada na makanisa mengine, jambo ambalo linakwamisha kuwekwa kwa baadhi ya vifaa vya ibada maalum kwa dhehebu lake katika kanisa hilo. [178]
vyema
Steve Mengere maarufu kwa jina la Stive Nyerere, anasema mwaka mpya wa 2009 ni mwaka wa mabadiliko kwake na anasema ni vyema kwa wasanii wenzake kuboresha kila kitu katika maisha kuanzia katika kazi za usanii, maisha, tabia na mavazi. [179]
vyuo
Akizungumzia kufunguliwa kwa vyuo hivyo Mukandala alisema majina ya wanafunzi waliotimiza masharti yote ya kudahiliwa upya tayari yameingizwa katika tovuti ya chuo hicho na kuwataka wanafunzi kuanza upya udahili kesho. [180]
waasi
Mwendesha mashtaka wa The Hegue, Petra Kneuer aliiambia mahakama hiyo kuwa badala ya kukabiliana na jeshi wanajeshi wa Bemba walikuwa wakiingia nyumba kwa nyumba na kuwabaka wanawake na wanaume,waliwaua na wengine kuwanyanyasa ili kuwatia hofu ya kuwaunga mkono waasi waliotaka kumpindua Patasse. [181]
wafuasi
Alisema kitendo hicho kimewafedhesha na kudai kwamba, askari hao walipigiwa simu na baadhi ya wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi wakidai kuwa chama hicho kinaleta vurugu. [182]
wako
Na ni vyema ukaongea naye ili upate ukweli kwa kusema wasiwasi wako, au kile ulichoambiwa kwa kumkutanisha na yule aliyesema itasaidia kuondoa migogoro yenu. [183]
walio
Ingawa hatua kadhaa tayari zimeanza kuchukuliwa na serikali ikiwamo kuwafikisha watuhumiwa wa kashfa hizo mahakamani lakini bado kuhusishwa kwa baadhi ya mawaziri walio madarakani, watendaji wa CCM na baadhi ya watendaji wa juu wa serikali na ufisadi, kunaonyesha kuwachosha wananchi, kukichafua chama hicho na kwamba kinahitaji kusafishwa. [184]
wanne
Siku hiyo tukiwa wanne tunatembea njiani mimi na kaka yangu na watu wengine wawili. [185]
wasiwasi
Na hili ndilo jambo linalowapa wasiwasi mkubwa wadau wa sekta hii muhimu katika maendeleo ya nchi. [186]
wawe
Awali, wanafunzi hao walitakiwa wawe wametimiza masharti ya udahili wao tangu Januari 2 mwaka huu. [187]
waweze
Alisema wameamua kuwarudisha wakacheze Tusker kwa mkopo ili waweze kulinda viwango vyao ambavyo vingeweza kushuka endapo wasingecheza mpira wa ushindani kwa muda mrefu. [188]
wenu
Wakati mwingine unaweza kukuta jambo kubwa mliligombania linakuwa dogo kutokana na uelewa wenu kwa kila moja wenu. [189]
wenzio
We Makengeza, pamoja na wenzio wote mnaopayuka magazetini mmechemsha kabisa. [190]
wiki
IKIWA imebaki wiki moja kufanyika uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Mbeya Vijijini, wenyeviti wa taifa wa vyama vya CUF, Tanzana Labour (TLP) na PPT Maendeleo, wamewasili mkoani Mbeya kuongeza nguvu katika kampeni za mgombea wa CUF, Daud Mponzi. [191]
yao
KAMATI ya Bunge ya Maliasili, Utalii na mazingira imewataka wakati wa kijiji cha Mayo Mayoka, wilayani Babati kuondoa hofu kuwa watahamishwa katika maeneo yao kutokana na bunge kuridhia upanuzi wa hifadhi ya Manyara. [192]
yapo
Akizungumza na Mwananchi jijini jana, Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega alisema mazungumzo baina ya timu hizo mbili yapo katika hatua ya awali, lakini alisema ana imani watafikia makubaliano. [193]
yenu
Inachokupasa ufahamu kuwa kuziba kauli katika suala ambalo limekuudhi hupelekea madhara makubwa mbeleni katika mahusiano yenu na huenda ikaathirika afya yako. [194]
za
Katika Jimbo la Moshi Vijijini la Dk Cyrill Chami, naibu waziri wa viwanda, biashara na masoko, kuna moshi unaofuka chini kwa chini baada Hans Mmasi aliyeshindwa na katika kura za maoni mwaka 2005 kurejea jimboni kufanya anachodai kutekeleza ahadi zake. [195]
zetu
Siyo kwamba hatutalitumia kanisa hilo, tutalitumia kwa ajili ya ibada za umoja na madhehebu mengine kama vile kuombea mvua na mambo mengineyo, lakini kwa ibada zetu za kawaida hatutaweza kulitumia kutokana na kanuni zetu za imani na taratibu za kuabudu kuwa tofauti na makanisa mengine," alieleza. [196]
zile
Afghanistan ni eneo linaloelezwa kuwa ni makutano ya nchi za Mashariki na zile za Magharibi, eneo maalum la kuanzia mapambano dhidi ya mataifa yasiyotabirika kama Iran, Iraq, Pakistan, India, China na mengineyo. [197]
zima
Viongozi wa UV-CCM hawakuweza kupatikana ili kuelezea juu ya mgeni huyo pamoja na suala zima la kongamano hilo ambalo linaonekana kuwa taarifa zake zimefanywa siri. [198]
zogo
Basi ikawa zogo, zogo kubwa kabisa hadi aliingia huyu huyu rafiki yangu aliyeonjeshwa mateso huko kwa Makaburu. [199]
zote
Mafunzo hayo ya siku 10 yaliyoshirikisha kata zote 13 za Manispaa ya Songea ambapo yalifikia kilele kwenye Ukumbi wa SACCOS ya walimu ya Songea vijijini, yametolewa na shirika lisilo la kiserikali la Self Help Development Community (SEDECO) kama njia mkakati ya kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI miongoni mwa vijana na jamii nzima kwa ujumla. [200]